Skip to main content

Posts

NAMNA YA KUANZA UPYA

  Kuanza upya ni jambo zuri ambalo linawezekana katika maeneo mengi ya maisha yetu, iwe ni kazi, uhusiano, au malengo binafsi. Hapa kuna hatua kadhaa unazoweza kuchukua kuanza upya: 1. Tathmini hali ya sasa Anza kwa kufanya tathmini ya hali yako ya sasa.  Jiulize maswali kuhusu maeneo gani unataka kuboresha au kubadilisha. Je, kuna mambo yanayokukwamisha au kukuzuia kufikia malengo yako? Kuelewa hali yako ya sasa ni hatua muhimu katika kuanza upya. 2. Weka malengo Weka malengo wazi na sahihi. Fikiria kwa kina kile unachotaka kufikia na kuamua hatua za kuifikia.  Malengo yako yanapaswa kuwa ya kusisimua, lakini pia yapaswa kuwa ya kufikika na yanayopimika.  Andika malengo yako na uwaeleze kwa uwazi. 3. Panga mpango wa utekelezaji Panga mpango wa vitendo wa jinsi utakavyotekeleza malengo yako. Tambua hatua ndogo na za kivitendo unazoweza kuchukua ili kufikia malengo yako.  Kwa kila hatua, weka muda uliopangwa na rasilimali zinazohitajika. 4. Jifunze kutokana na uz...

#NAJIFUNZA_05: MAARIFA SAHIHI NA YA KUTOSHA KWA MAFANIKIO YAKO

 George Bernard Shaw aliwahi kusema maneno haya......"beware of false knowledge, it is more dangerous than ignorance" Kwamba "Kuwa makini sana na taarifa zisizo sahihi,  kwa sababu ni hatari zaidi kuliko ujinga" Taarifa ni kitu cha msingi sana, unapohitaji kufanya jambo fulani. Ukweli ni kuwa unahitajika kuwa na taarifa nyingi, kabla ya kufanya jambo. Lakini taarifa hizo lazima ziwe sahihi sana, kwa sababu zisipokuwa  sahihi zitakupelekea mahali pabaya. Ili ufanye vyema katika jambo fulani, unalazimika kuwa na taarifa nyingi na zilizo sahihi. Kuwa makini sana na vyanzo vya taarifa yako Fanyia tathmini kwanza, juu ya chanzo cha taarifa, Je, ni sahihi na zitakufaa. Kumbuka, Maamuzi yoyote yale yanategemea taarifa ulizo nazo. Kufeli au kufanikiwa kunategemea na taarifa ulizo nazo. Kiwango cha usahihi wa taarifa huamua aina ya matokeo ambao unakwenda kuyapata. ..Wito wangu ni kuwa, tuko katika karne ya TAARIFA, karne ambayo walio na taarifa sahihi ndio wanaofanikiwa. Na...

KUTOKA VITABUNI 01_KILA KITU KINA MAANA KULINGANA NA MAANA YA MHUSIKA

  You give a meaning to every thing you see. Nimekuwa nikisema kuwa, hakuna kitu kibaya au kizuri, ila mtazamo wako ndio unaweza fanya hivyo. Namna ambavyo wewe unalitazama jambo fulani, ndivyo linavyokuwa na namna hiyo, na haitaweza kufanana na mwingine. Mtu fulani ni mzuri au mbaya kulingana na namna ambavyo unavyomtazama. Leo nakuambia kuwa, Kila kitu kinapewa tafsiri na wewe. Hakiwi kizuri au kibaya, ila ni kwamba namna ambayo wewe umetoa tafsiri au maana hiyo. Jambo laweza kutokea hapa na kushuhudiwa na watu wawili, kila mmoja akalipa maana yake. Hivyo unavyosema jambo fulani ni zuri au baya ni kwa namna tu wewe uonavyo na si wote wanaona hivyo. Usemavyo tu fulani anafaa au hafai, ni namna tu ambavyo wewe umemtafsiri na sio wote wamemtafsiri hivyo. Tafsiri au maana ya jambo ulipalo wewe, kamwe halitafanana na mtu mwingine. Ni wewe uonavyo hivyo, sio wote tunaona hivyo. Wamuona mtu fulani ni mbaya, ni vile  wewe unaona hivyo na sio wote. Usituaminishe au kutuambukiza tafsi...

MAKALA 01; RAFIKI BORA NI VITABU (THE BEST FRIEND IS BOOKS)

  MAKALA 01; RAFIKI BORA NI VITABU (THE BEST FRIEND IS BOOKS)   Habari yako rafiki yangu, Ni matumaini yangu kwamba u mzima wa afya kabisa, Karibu katika mfulululizo wa makala hizi kutoka katika kitengo cha KUTOKA VITABUNI, Ili kuweza kuwa bora katika maisha yako ni vyema sana ukaambatana na kuzungukwa na watu walio na kile ambacho wewe unataka kuwa. Ni asilimia 85% ya mafanikio yako huchangiwa na watu wanaokuzunguka.   Marafiki zako, ndugu zako na jamaa zako ambao unatumia muda mwingi kuwa nao kazini, shuleni, ofisini na maeneo mbalimbali ni muhimu wakachunguzwa na kuona kama wanaweza kukupeleka kule ambako unataka kufika. Upo msemo wa Kiswahili ambao huzungumzwa kwamba ukitembea na mwizi na wewe utakuwa mwizi, hii humaanisha kwamba ukiambatana na mtu mwenye tabia Fulani,automatically kuna baadhi ya mambo ambayo utayavuta kutoka kwa rafiki yako. Eneo hili ni muhimu sana kwa sababu linachangia kwa kiwango kikubwa katika mafanikio yetu na katika safari ya kufika ku...

MY MEMORIES _MY BRAIN REMEMBER THIS

  MY MEMORIES _MY BRAIN REMEMBER THIS . Wakati nikiwa mdogo sana, nilijiona nikiwa mwalimu mkubwa sana na mwenye maisha fulani mazuri. Wakati mwingine nilikuwa na ndoto za kuwa daktari bingwa (Specialization). Ambapo kwa mara ya kwanza nilitamani sana kuwa Daktari aliyebobea kwenye masuala ya kutibu meno. Nikiwa naanza Kidato cha kwanza, wazo la ualimu liliendelea kuishi ndani yangu hadi kidato cha tatu, ambapo nilibadili wazo hilo na kuanza kufikiri kuwa Mhandishi wa Barabara (Civil Engineering) na nikaanza kuongeza juhudi kabisa katika Hesabu ili niweze kufanya vizuri katika hesabu na kupata nafasi ya kwenda kusomea Mchepuo wa PCM. Na ninachokumbuka ni kwamba katika mawazo yote hayo niliyokuwa na ndoto nilizokuwa nazo, nilipenda sana kuwaelekeza wengine pale ambapo hawaelewi na wakati mwingine kujipendekeza kuelekeza hata kama sijaombwa kufanya hivyo. Lakini baadaye kidogo (Mwishoni mwa Kidato cha nne), Nikawaza kuwa Daktari wa Masikio na wazo hili alilirudia mama yangu, baada ya...

ANZA SASA, UMRI USIWE KIKWAZO CHA WEWE KUTOTIMIZA NDOTO ZAKO

 ANZA SASA KUFANYA, UMRI ISIWE KIKWAZO KWAKO. Bila shaka unayo maono fulani (Unajiona ukiwa unafanya kitu baadaye ambacho ni kikubwa sana). Kwa namna fulani unatambua jambo fulani unaweza kulifanya kwa ufanisi mkubwa kabisa. Na unajua kabisa, kwamba utakapofanya jambo lile utakuwa katika viwango fulani vikubwa sana. Lakini, mbona huanzi? Nini kinakukwamisha usiendelee?  Ni ujuzi, Maarifa, huelewi pa kuanzia? Au unasema ngoja nikue kidogo au nifikie hatua fulani?. Tuko watu ambao tunasubiri hadi tufike viwango fulani vya Elimu ndipo tuanze kutumiza ndoto zetu. Tuko watu tunaosubiri tufikie Umri fulani ili tuanze kutimiza ndoto zetu. Lakini tunajichelewesha wenyewe, umri sio tatizo kabisa. Kwani haujaona Watu wakiwa na Umri mdogo na wanafanya Makubwa?. Je, Mastaa wengi katika tasnina mbalimbali duniani wana Miaka mingapi hadi muda huu na walianza wakiwa na Miaka mingapi? Je, Mabilionea wa Dunia wana Miaka mingapi muda huu?. Je unamfahamu Rev Victor Githu  kutoka Kenya ...

KARIBU KATIKA PROGRAM YA ELIMU KITAA(LEARNING SITE)

  Elimu Kitaa Foundation inakukakaribisha Katika Program ya Elimu Kitaa Habari ya kwako rafiki yangu. Bila shaka uko vizuri na unaendelea vyema na majukumu ya kila siku. Naitwa Joshua Golyama  mwanafunzi wa Shahada ya awali ya Sayansi ya Kilimo kwa Ujumla(Bsc.Agriculture General) kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine Cha Kilimo (SUA                                         Mwanzilishi wa Program inayoitwa ELIMU KITAA. Leo ninapenda kukuletea maeneo mbalimbali ambayo unaweza yatembelea na tukajifunza pamoja na mimi. Maeneo hayo utapata nafasi ya kusoma makala ambazo ninaziandika kila siku na kuziweka humo, na tukajifunza kwa pamoja na kupata maarifa zaidi na zaidi. Kwanza kabisa nikupe utangulizi wa maana halisi ya Neno hili ELIMU KITAA. Elimu Kitaa ni program inayohusika na kuandika makala mbalimbali katika mitandao ya Kijamii na kuandaa semina mbalimbali zenye kutupa maarifa muhimu san...

JENGA TABIA YA KUJIFUNZA KILA WAKATI , ONDOA KIBURI KATIKA KUJIFUNZA.

JENGA TABIA YA KUJIFUNZA KILA WAKATI ,  ONDOA KIBURI KATIKA KUJIFUNZA. Unapokosa tabia ya kujifunza na kuwa na hali ya kujiona unajua kila kitu utakuwa nayo na Kwa Maana Hiyo hautaweza kuwa na spirit ya kuendelea kujifunza zaidi na zaidi. Lakini unapokuwa unajifunza kila wakati, utagundua kwamba Mambo mengi huyajui hii itaamusha Nguvu mpya, ari mpya na hamasa ya kue ndelea kujifunza zaidi. Jifunze zaidi ili upate hamasa ya kujifunza zaidi. Na MUHIMU,  ili uweze kujifunza ni lazima ujione hujui , na kama utaona kama unajua kamwe hautaweza kujifunza Kwa maneno Mengine unakuwa na KIBURI KATIKA KUJIFUNZA ambacho Kinakuzuia wewe kujifunza zaidi, kwa sababu ndani yako kutakuwa na Sauti kama hii  'mbona kila kitu ninakijua, kujifunza ni kupoteza muda' Hakikisha unajitahidi unakuwa na Tabia Ya KUJIFUNZA, kwa sababu katika Karne hii Ya 21 kuna Maendeleo makubwa sana Ya Teknolojia na Ni ULIMWENGU WA TAARIFA hivyo usipojifunza kamwe hauwezi kuwa na Taarifa sa...

HEKIMA YA SIKU; Kila Jambo ulifanyalo lifanye kama wajibu na si kutegemea shukrani au kutambulika

Kila jambo unalolifanya, lifanye kama wajibu, na usifanye ukitegemea kutambuliwa, au kupewa shukrani. Watu wengi  wanapata shida sana  pale ambapo wanafanya mambo mengi, na hakuna anayeonekana kuwashukuru kwa yale wanayoyafanya. Unajitoa kwa nguvu zako kuhakikisha kila kitu kinakuwa sawa. Fuatilia mifano hii michache ili uweze kupata kile ninachokimaanisha hapa; Mfano  wa kwanza; Viongozi mbalimbali tulio nao, wanatumia muda wao mwingi na nguvu nyingi kuhakikisha wale wanaowaongoza wanafika pale wanapotakiwa kuwa. Na  hakuna hata mmoja anayetambua mchango wao na nguvu zao walizotumia kuwaongoza. Na pengine asiwepo hata mmoja wa kusema asante kwa yale wanayafanya. Mfano wa Pili ; kwenye mahusiano,unakuta boyfriend/girlfriend anafanya kila anachoweza ili kuboresha mahusiano yao, kumsaidia kwa kila hali/changamoto anayoipitia Lakini haoni mwenzie akimshukuru au kutambua kwa kile anakifanya. Mfano wa tatu; Kazini kwako, unafanya kila kitu vile inavyotaki...

KUWA MAKINI SANA NA NAMNA UNAVYOTUMIA MUDA WAKO

KUWA MAKINI SANA NA NAMNA UNAVYOTUMIA MUDA WAKO "Muda ni wa thamani sana kuliko fedha , unaweza kuzipata fedha kila siku Lakini muda hauwezi kuupata ukishaupoteza. Hivyo, tunatakiwa muda vizuri ule tunaoupata na kwa umakini mkubwa zaidi. Epuka kupoteza muda kwa kutofanya yale yasiyo na umuhimu kwako. Maana wengi tunahangaika na mambo mengi sana ambayo hayana mchangi wowote katika maisha yetu. Pale upatapo nafasi ya kufanya jambo, hakikisha unalikamilisha na kwa usahihi kabla ya kuanza kufanya jambo jingine. Wekeza muda wako kwa kujifunza zaidi , wekeza zaidi ndani yako, ilishe akili yako maarifa mapya kila siku ili kuweza kuwa na mabadiliko makubwa hapo baadaye. Wekeza ndani yako kwa kusoma vitabu, kusoma Makala na kuhudhuria semina mbalimbali Jifunze kila siku na hii ni ni namna sahihi ya kutumia muda wako Vizuri. Huwa napenda kusema kuwa, watu wengi tunalalamika na kukiri kwamba " muda mchache , na Mambo mengi, Swali langu ni hili Je,  hayo Mengi uliyo nayo...

KITABU CHA JUMA; My Philosphy For Successful Living -Falsafa Yangu Ya Maisha Ya Mafanikio.

KITABU CHA JUMA; My Philosphy For Successful Living -Falsafa Yangu Ya Maisha Ya Mafanikio. Habari ya kwako rafiki mpendwa, Natumai umekuwa na wiki ya baraka sana na bila shaka umepiga hatua kadhaa zenye kukusaidia katika safari hii tuliyonayo ya kulikamilisha kusudi la Mungu katika maisha yetu. Nikukaribishe katika makala hii ya kitabu cha Juma,  kutoka katika Kitabu Cha My Philosophy For Successful Living-Falasafa yangu ya Maisha Ya Mafanikio kilichoandikwa na Jim Rohn Jim Rohn ni Mjasiriamali wa Marekani, Mwandishi, na mhamasishaji Katika Juma hili tunakwenda kujifunza mambo machache na ya muhimu sana kutoka katika Kitabu hiki  cha My Philosophy For successful living Karibu sana tujifunze kwa pamoja mambo haya ambayo mwandishi anatufundisha katika kitabu hiki Kila mmoja wetu anatamani kuwa na maisha mazuri, hakuna hata mmoja anayetamani kuishi maisha ya shida. Lakini kutokana na ujinga wetu wa kutofahamu kanuni za Msingi za kuwa na maisha mazuri tunaishia k...

KUTOA KAFARA ILI UWEZE KUWA NA MAFANIKIO MAKUBWA.

Bila shaka kichwa cha mada hii kinakuchanganya na unashindwa kuelewa nini nimedhamiria  kukuambia, Lakini ambatana nami hadi mwisho mwa Makala hii utaelewa maeneo halisi ya mada hii ya leo. Karibu sana tujifunze pamoja ili tupate Maarifa ya kutusaidia. Wakati naendelea kusoma vitabu mbalimbali, nilikutana na jambo hili ambalo lilinishangaza kidogo, lakini nilijifunza mambo mengi sana muhimu katika safari ya mafanikio. Nimeyasoma na kujifunza kutoka kitabu cha K WANINI HADI WEWE SIO TAJIRI   kilichoandikwa na Kocha Makirita Amani Nimeamua nikushirikishe maarifa haya nawe upate kujifunza , na kuchukua hatua ya kuyafanyia kazi. Mwandishi anaanza kwa kueleza yafuatayo;  Huwezi kufikia utajiri mkubwa na mafanikio kwenye maisha bila ya KUTOA KAFARA. Mwandishi anaeleza dhana ya TRADE OFF akiwa na maana kwamba " Kupoteza kitu fulani ili kupata kitu kingine , au kuliwa eneo fulani ili uweze kula eneo jingine  Kafara anayozungumzia mwandishi...

KITABU CHA JUMA; My philosophy for successful living-Falsafa Yangu ya Maisha Ya Mafanikio Kilichoandikwa na Jim Rohn

KITABU CHA JUMA;  My philosophy for successful living- Falsafa Yangu ya Maisha Ya Mafanikio  Kilichoandikwa na Jim Rohn. Moja ya jambo muhimu sana katika dunia hii ya sasa ni kujifunza, ili kuweza kuwa bora zaidi katika jambo lolote huna budi kuwa na tabia ya kujifunza,  Kupitia kujifunza tunapata maarifa ambayo yanaweza kutuvusha hatua moja kwenda hatua nyingine. Kufikia mafanikio makubwa sana katika maisha hatuna budi kujifunza kila siku Watu wengi ambao wamefanikiwa wana tabia moja muhimu sana ambayo ni Kujifunza kila wakati na kila siku, shauku yao kubwa ni kujfunza na kujua mambo mengi ambayo yanawasaidia kukua zaidi  Kupitia kujifunza, unapata nafasi ya kuyajua mambo mengi sana katika maisha.Hatuwezi kuyajua yote lakini tunatakiwa kujua mambo mengi. Kama utapata nafasi ya kuwafutilia sana wale wanaojua mambo mengi katika Jamii , wana tabia ya kujifunza kila siku na kila wakati. Hivyo, kama tunataka kufikia mafanikio makubw...

KARIBU KATIKA MTANDAO WA ELIMU KITAA (STREET EDUCATION); Tujifunze kwa pamoja, ili tupate maarifa sahihi ya kutusaidia katika maisha yetu.

                                                  Rafiki yangu mpendwa; Ni matumaini yangu kuwa unaendelea vizuri na majukumu ya kila siku na unaendelea kufanya kazi kwa bidi ili kuwa na maisha bora sana. Moja ya kitu cha msingi sana katika maisha ambacho hutakiwi kukiacha ni kujifunza kila siku na kutafuta kuwa bora zaidi. Maisha ni sanaa, na kama ilivyo sanaa inahitaji ubunifu kila siku, usipotaka kujifunza kamwe hauwezi kuwa mbunifu. Hivyo, katika maisha hutakiwi kuacha kujifunza ili uweze kuwa bora zaidi. Karibu sana katika Makala hii ambayo ni muhimu sana kwako na nimeifanya kuwa maalumu sana, kwa sababu nimekuandalia na kukuletea Makala hii ili uweze kujua hasa kwa undani kuhusu Mtandao huu wa Elimu KItaa (Street Education) chanzo chake, unahusika na nini, malengo yake na nini utakipata katika mtandao huu. Karibu s...

KURASA 05; KUJITAMBUA, Na umuhimu wake katika maisha ya kila siku

" Kujitambua"  maana  yake  nini?? Unaelewa  nini  kuhusiana  na  neno Hili Kujitambua?. ' Kujitambua '  limetokana  na  neno Tambua lenye maana ya kujua/kuelewa Hivyo; Kujitambua ni hali ya mtu binafsi kujielewa vile alivyo. Au uwezo wa mtu binafsi kung'amua yeye ni nani?, Anapaswa kufanya nini na kwa sababu ipi na lini? Pia, Kujitambua ni uwezo wa mtu  binafsi  kujielewa vizuri kuhusu yeye, tabia zake , majibu yake na vyote vile ambavyo vinamzunguka.  Katika suala hili ya kujitambua , mtu huyu lazima aweze kuyaelewa mambo yafuatayo kuhusu yeye ;  Yeye ni nani? (Mimi ni nani?) Uwezo wake (wako binafsi) ni upi?  Hapa naamanisha (upekee wako ulionao ) kunakopelekea utofauti wako na watu wengine Nini  natakiwa kukifanya hapa duniani? Unaelekea wapi ? Mchango wako  kwa jamii inayokuzunguka ni upi?? 👆 hayo ni mambo ambayo mtu anayejitambua ana...