You give a meaning to every thing you see.
Nimekuwa nikisema kuwa, hakuna kitu kibaya au kizuri, ila mtazamo wako ndio unaweza fanya hivyo.
Namna ambavyo wewe unalitazama jambo fulani, ndivyo linavyokuwa na namna hiyo, na haitaweza kufanana na mwingine.
Mtu fulani ni mzuri au mbaya kulingana na namna ambavyo unavyomtazama.
Leo nakuambia kuwa, Kila kitu kinapewa tafsiri na wewe.
Hakiwi kizuri au kibaya, ila ni kwamba namna ambayo wewe umetoa tafsiri au maana hiyo.
Jambo laweza kutokea hapa na kushuhudiwa na watu wawili, kila mmoja akalipa maana yake.
Hivyo unavyosema jambo fulani ni zuri au baya ni kwa namna tu wewe uonavyo na si wote wanaona hivyo.
Usemavyo tu fulani anafaa au hafai, ni namna tu ambavyo wewe umemtafsiri na sio wote wamemtafsiri hivyo.
Tafsiri au maana ya jambo ulipalo wewe, kamwe halitafanana na mtu mwingine.
Ni wewe uonavyo hivyo, sio wote tunaona hivyo.
Wamuona mtu fulani ni mbaya, ni vile wewe unaona hivyo na sio wote.
Usituaminishe au kutuambukiza tafsiri au maana ya kitu fulani uliyo nayo wewe.
Usituambize chuki uliyo nayo kwa mtu mwingine, kwa kuwa sivyo mwingine aonavyo.
Ndivyo maisha yalivyo, kila mmoja na maana yake.
You give meaning to everythiny you see
©Kiss That Frog.
Unaweza jifunza zaidi kwa kusoma.
1. Kitabu kifupi nilichoandika kwa kugusa maneno haya hapa chini RAFIKI BORA NI KITABU bila shaka utajifunza na kubarikiwa zaidi.
Makala hii imeandikwa na;
Joshua Golyama
(Mwandishi, Mwalimu, Blogger na Mwazilishi wa Taasisi ya Elimu Kitaa Foundation).
Mawasiliano; +255 764 257 495/ +255 622 163 323.
Baruapepe;golyamajoshua@gmail.com auelimukitaa2020@gmail.com
Comments
Post a Comment