Skip to main content

Posts

Featured Post

NAMNA YA KUANZA UPYA

  Kuanza upya ni jambo zuri ambalo linawezekana katika maeneo mengi ya maisha yetu, iwe ni kazi, uhusiano, au malengo binafsi. Hapa kuna hatua kadhaa unazoweza kuchukua kuanza upya: 1. Tathmini hali ya sasa Anza kwa kufanya tathmini ya hali yako ya sasa.  Jiulize maswali kuhusu maeneo gani unataka kuboresha au kubadilisha. Je, kuna mambo yanayokukwamisha au kukuzuia kufikia malengo yako? Kuelewa hali yako ya sasa ni hatua muhimu katika kuanza upya. 2. Weka malengo Weka malengo wazi na sahihi. Fikiria kwa kina kile unachotaka kufikia na kuamua hatua za kuifikia.  Malengo yako yanapaswa kuwa ya kusisimua, lakini pia yapaswa kuwa ya kufikika na yanayopimika.  Andika malengo yako na uwaeleze kwa uwazi. 3. Panga mpango wa utekelezaji Panga mpango wa vitendo wa jinsi utakavyotekeleza malengo yako. Tambua hatua ndogo na za kivitendo unazoweza kuchukua ili kufikia malengo yako.  Kwa kila hatua, weka muda uliopangwa na rasilimali zinazohitajika. 4. Jifunze kutokana na uz...
Recent posts

#NAJIFUNZA_05: MAARIFA SAHIHI NA YA KUTOSHA KWA MAFANIKIO YAKO

 George Bernard Shaw aliwahi kusema maneno haya......"beware of false knowledge, it is more dangerous than ignorance" Kwamba "Kuwa makini sana na taarifa zisizo sahihi,  kwa sababu ni hatari zaidi kuliko ujinga" Taarifa ni kitu cha msingi sana, unapohitaji kufanya jambo fulani. Ukweli ni kuwa unahitajika kuwa na taarifa nyingi, kabla ya kufanya jambo. Lakini taarifa hizo lazima ziwe sahihi sana, kwa sababu zisipokuwa  sahihi zitakupelekea mahali pabaya. Ili ufanye vyema katika jambo fulani, unalazimika kuwa na taarifa nyingi na zilizo sahihi. Kuwa makini sana na vyanzo vya taarifa yako Fanyia tathmini kwanza, juu ya chanzo cha taarifa, Je, ni sahihi na zitakufaa. Kumbuka, Maamuzi yoyote yale yanategemea taarifa ulizo nazo. Kufeli au kufanikiwa kunategemea na taarifa ulizo nazo. Kiwango cha usahihi wa taarifa huamua aina ya matokeo ambao unakwenda kuyapata. ..Wito wangu ni kuwa, tuko katika karne ya TAARIFA, karne ambayo walio na taarifa sahihi ndio wanaofanikiwa. Na...

KUTOKA VITABUNI 01_KILA KITU KINA MAANA KULINGANA NA MAANA YA MHUSIKA

  You give a meaning to every thing you see. Nimekuwa nikisema kuwa, hakuna kitu kibaya au kizuri, ila mtazamo wako ndio unaweza fanya hivyo. Namna ambavyo wewe unalitazama jambo fulani, ndivyo linavyokuwa na namna hiyo, na haitaweza kufanana na mwingine. Mtu fulani ni mzuri au mbaya kulingana na namna ambavyo unavyomtazama. Leo nakuambia kuwa, Kila kitu kinapewa tafsiri na wewe. Hakiwi kizuri au kibaya, ila ni kwamba namna ambayo wewe umetoa tafsiri au maana hiyo. Jambo laweza kutokea hapa na kushuhudiwa na watu wawili, kila mmoja akalipa maana yake. Hivyo unavyosema jambo fulani ni zuri au baya ni kwa namna tu wewe uonavyo na si wote wanaona hivyo. Usemavyo tu fulani anafaa au hafai, ni namna tu ambavyo wewe umemtafsiri na sio wote wamemtafsiri hivyo. Tafsiri au maana ya jambo ulipalo wewe, kamwe halitafanana na mtu mwingine. Ni wewe uonavyo hivyo, sio wote tunaona hivyo. Wamuona mtu fulani ni mbaya, ni vile  wewe unaona hivyo na sio wote. Usituaminishe au kutuambukiza tafsi...

MAKALA 01; RAFIKI BORA NI VITABU (THE BEST FRIEND IS BOOKS)

  MAKALA 01; RAFIKI BORA NI VITABU (THE BEST FRIEND IS BOOKS)   Habari yako rafiki yangu, Ni matumaini yangu kwamba u mzima wa afya kabisa, Karibu katika mfulululizo wa makala hizi kutoka katika kitengo cha KUTOKA VITABUNI, Ili kuweza kuwa bora katika maisha yako ni vyema sana ukaambatana na kuzungukwa na watu walio na kile ambacho wewe unataka kuwa. Ni asilimia 85% ya mafanikio yako huchangiwa na watu wanaokuzunguka.   Marafiki zako, ndugu zako na jamaa zako ambao unatumia muda mwingi kuwa nao kazini, shuleni, ofisini na maeneo mbalimbali ni muhimu wakachunguzwa na kuona kama wanaweza kukupeleka kule ambako unataka kufika. Upo msemo wa Kiswahili ambao huzungumzwa kwamba ukitembea na mwizi na wewe utakuwa mwizi, hii humaanisha kwamba ukiambatana na mtu mwenye tabia Fulani,automatically kuna baadhi ya mambo ambayo utayavuta kutoka kwa rafiki yako. Eneo hili ni muhimu sana kwa sababu linachangia kwa kiwango kikubwa katika mafanikio yetu na katika safari ya kufika ku...

MY MEMORIES _MY BRAIN REMEMBER THIS

  MY MEMORIES _MY BRAIN REMEMBER THIS . Wakati nikiwa mdogo sana, nilijiona nikiwa mwalimu mkubwa sana na mwenye maisha fulani mazuri. Wakati mwingine nilikuwa na ndoto za kuwa daktari bingwa (Specialization). Ambapo kwa mara ya kwanza nilitamani sana kuwa Daktari aliyebobea kwenye masuala ya kutibu meno. Nikiwa naanza Kidato cha kwanza, wazo la ualimu liliendelea kuishi ndani yangu hadi kidato cha tatu, ambapo nilibadili wazo hilo na kuanza kufikiri kuwa Mhandishi wa Barabara (Civil Engineering) na nikaanza kuongeza juhudi kabisa katika Hesabu ili niweze kufanya vizuri katika hesabu na kupata nafasi ya kwenda kusomea Mchepuo wa PCM. Na ninachokumbuka ni kwamba katika mawazo yote hayo niliyokuwa na ndoto nilizokuwa nazo, nilipenda sana kuwaelekeza wengine pale ambapo hawaelewi na wakati mwingine kujipendekeza kuelekeza hata kama sijaombwa kufanya hivyo. Lakini baadaye kidogo (Mwishoni mwa Kidato cha nne), Nikawaza kuwa Daktari wa Masikio na wazo hili alilirudia mama yangu, baada ya...

ANZA SASA, UMRI USIWE KIKWAZO CHA WEWE KUTOTIMIZA NDOTO ZAKO

 ANZA SASA KUFANYA, UMRI ISIWE KIKWAZO KWAKO. Bila shaka unayo maono fulani (Unajiona ukiwa unafanya kitu baadaye ambacho ni kikubwa sana). Kwa namna fulani unatambua jambo fulani unaweza kulifanya kwa ufanisi mkubwa kabisa. Na unajua kabisa, kwamba utakapofanya jambo lile utakuwa katika viwango fulani vikubwa sana. Lakini, mbona huanzi? Nini kinakukwamisha usiendelee?  Ni ujuzi, Maarifa, huelewi pa kuanzia? Au unasema ngoja nikue kidogo au nifikie hatua fulani?. Tuko watu ambao tunasubiri hadi tufike viwango fulani vya Elimu ndipo tuanze kutumiza ndoto zetu. Tuko watu tunaosubiri tufikie Umri fulani ili tuanze kutimiza ndoto zetu. Lakini tunajichelewesha wenyewe, umri sio tatizo kabisa. Kwani haujaona Watu wakiwa na Umri mdogo na wanafanya Makubwa?. Je, Mastaa wengi katika tasnina mbalimbali duniani wana Miaka mingapi hadi muda huu na walianza wakiwa na Miaka mingapi? Je, Mabilionea wa Dunia wana Miaka mingapi muda huu?. Je unamfahamu Rev Victor Githu  kutoka Kenya ...

KARIBU KATIKA PROGRAM YA ELIMU KITAA(LEARNING SITE)

  Elimu Kitaa Foundation inakukakaribisha Katika Program ya Elimu Kitaa Habari ya kwako rafiki yangu. Bila shaka uko vizuri na unaendelea vyema na majukumu ya kila siku. Naitwa Joshua Golyama  mwanafunzi wa Shahada ya awali ya Sayansi ya Kilimo kwa Ujumla(Bsc.Agriculture General) kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine Cha Kilimo (SUA                                         Mwanzilishi wa Program inayoitwa ELIMU KITAA. Leo ninapenda kukuletea maeneo mbalimbali ambayo unaweza yatembelea na tukajifunza pamoja na mimi. Maeneo hayo utapata nafasi ya kusoma makala ambazo ninaziandika kila siku na kuziweka humo, na tukajifunza kwa pamoja na kupata maarifa zaidi na zaidi. Kwanza kabisa nikupe utangulizi wa maana halisi ya Neno hili ELIMU KITAA. Elimu Kitaa ni program inayohusika na kuandika makala mbalimbali katika mitandao ya Kijamii na kuandaa semina mbalimbali zenye kutupa maarifa muhimu san...