KITABU CHA JUMA; My philosophy for successful living-Falsafa Yangu ya Maisha Ya Mafanikio Kilichoandikwa na Jim Rohn
KITABU CHA JUMA; My philosophy for successful living-Falsafa Yangu ya Maisha Ya Mafanikio Kilichoandikwa na Jim Rohn.
Moja ya jambo muhimu sana katika dunia hii ya sasa ni kujifunza, ili kuweza kuwa bora zaidi katika jambo lolote huna budi kuwa na tabia ya kujifunza,
Kupitia kujifunza tunapata maarifa ambayo yanaweza kutuvusha hatua moja kwenda hatua nyingine. Kufikia mafanikio makubwa sana katika maisha hatuna budi kujifunza kila siku
Watu wengi ambao wamefanikiwa wana tabia moja muhimu sana ambayo ni Kujifunza kila wakati na kila siku, shauku yao kubwa ni kujfunza na kujua mambo mengi ambayo yanawasaidia kukua zaidi
Kupitia kujifunza, unapata nafasi ya kuyajua mambo mengi sana katika maisha.Hatuwezi kuyajua yote lakini tunatakiwa kujua mambo mengi.
Kama utapata nafasi ya kuwafutilia sana wale wanaojua mambo mengi katika Jamii , wana tabia ya kujifunza kila siku na kila wakati.
Hivyo, kama tunataka kufikia mafanikio makubwa na kufanya mambo kwa ubora hatuna budi ya kujifunza kila siku
Kama tunataka kuyajua mambo mengi katika dunia hii, hatuna budi kujifunza kila siku.
Zipo njia mbalimbali ambazo tunaweza kuzitumia ili kujifunza,
Lakini leo ninakushirikisha njia moja ambayo ni Kujifunza kupitia Kusoma Vitabu.
Maarifa mengi yamefichwa kwenye vitabu.
Waandishi wa vitabu wameyashirikisha maarifa waliyokuwa kwa kuandika vitabu.
Kupitia kusoma vitabu tunapata maarifa mengi ya kujifunza, kufahamu mambo mbalimbali kuhusiana na vitu ambavyo tunatamani kuvijua.
Hivyo, ni vyema sana kusoma vitabu hasa vinavyotoa maarifa sahihi kuhusiana na kile unachotaka kukifahamu.
Soma vitabu vile vinahusiana na kazi yako, biashara yako, na chochote kile unachohitaji kukifahamu.
Moja ya jambo ambalo ninalolifanya katika blogu hii ni kuhamasisha kusoma vitabu na kushirikisha yale ambayo tunajifunza kupitia kusoma.
Hivyo, basi kwa Juma hili tutakuwa na kitabu kizuri sana ambacho tutakwenda kujifunza,
Kinachoitwa My philosophy for Successful Living Falsafa Yangu ya Maisha Ya Mafanikio Kilichoandikwa na Jim Rohn.
Kitabu hiki kina mambo mengi sana ambayo kama tutayasoma na kuyachukua tunakwenda kuwa na mafanikio makubwa sana.
Yaliyoandikwa humo ni maarifa aliyoyapata mwandishi katika safari ya kujifunza kuhusu maisha ya mafanikio.
Kitabu hiki kina kurasa 25 tu, kina Sura saba na ambazo ni fupi sana, najua hutashindwa kuzisoma.
Kwa juma hili lote, tutakuwa tukisoma kitabu hiki na kila mmoja aliyepata nafasi ya kukisoma ataruhusiwa kuchangia kile alichojifunza,
Na mwisho wa Juma hili utapata Makala Kamili Ya Uchambuzi wa Kitabu wa hiki..
Mambo machache ambayo tutakwenda kujifunza kutoka katika kitabu hiki cha Juma ni haya yafuatayo;
1. Muda ni wa thamani sana kuliko fedha, unaweza kupata fedha za kutosha , lakini hauwezi kupata muda wa kutosha.
Mwandishi anatupa ushauri wa kutumia muda wetu tulio nao kwa Hekima na kwa umakini mkubwa kwa sababu muda ukishapita hauwezi kurudi tena.
2. Elimu ya Darasani(Formal education) inakusaidia kupata ajira, lakini Elimu binafsi(self-education) ndiyo inayoweza kukufanya kuwa tajiri.
3. Falsafa ya Kuzalisha zaidi na kufanya vizuri zaidi(Performance).
Siri kubwa ya mafanikio imefichwa katika kuwasaidia wengine.
Tafuta kila njia kuwatumikia/kuwasaidia wengine kufikia malengo yao.
4. Fedha ni 'mchezo wa thamani' Kadiri unavyotoa thamani , ndivyo unavyoweza kupata fedha zaidi.
Ili kupata fedha zaidi, tafuta zaidi kuongeza thamani katika kile unachokifanya.
5. Ujue Msingi wa mafanikio yako na unatakiwa kuimarisha(fundamentals)
Kila kitu kina msingi wake(foundation), na msingi ukiwa Imara ndivyo unaweza kuendelea na kuimarika zaidi.
6. Chagua watu sahihi wa kushirikiana na wewe katika safari ya mafanikio au katika jambo ambalo umekusudia kulifanya.
Hautafanya peke yako, unahitaji watu wa kuambatana na wewe , hivyo unatakiwa kuwa makini na katika kuchagua wale unaotaka kuambatana nao.
7. Boresha na Imarisha falsafa yako binafsi ambayo umejitengenezea.
Katika maisha haya unapaswa kuwa na Falsafa yako ambayo itakuongoza katika maisha yako.Na unatakiwa kuiboresha na kuifanya imara kila wakati.
8. Namna ya kufikia uhuru wa kifedha na kuondokana na madeni,
Kuwa na madeni ni utumwa, na yanaweza kukuzuia kutofika kule unakotaka kufika.
️9. Mambo sita muhimu ya kufanya ili uweze kuwa maisha bora(yasiyo ya kawaida-kiwango cha juu zaidi)
Extraordinary life.
Hayo ni mambo machache ambayo tutakwenda kujifunza kutoka katika kitabu hiki cha Juma
Hivyo nikukaribishe na nikuhamasishe uweze kukisoma kitabu hiki na kufuatilia uchambuzi wake, najua tunakwenda kujifunza mambo mengi sana kutoka katika kitabu hiki.
Karibu sana tujumuike kwa pamoja kujifunza.
Uchambuzi wa kitabu hiki kwa undani zaidi, utapata katika group la Whatsap la Elimu Ya Kitaa .
Kujiunga na group la whatsap la Elimu Kitaa tuma Sms Kwa njia ya whatsap ikiwa na Jina Lako na Neno NIUNGE ELIMU KITAA nawe utaunganishwa. Mfano; Joshua Golyama, NIUNGE ELIMU KITAA
Wako Joshua Golyama
Ahsante sana
_____________________________________________
Makala hii imeandaliwa na kuandikwa na;
Joshua Golyama, ambaye ni mwanafunzi Kutoka Chuo Kikuu Cha Sokoine Cha Kilimo(SUA-MOROGORO), Mhamasishaji wa Mafanikio na Mwandishi.
Comments
Post a Comment