Bila shaka kichwa cha mada hii kinakuchanganya na unashindwa kuelewa nini nimedhamiria kukuambia, Lakini ambatana nami hadi mwisho mwa Makala hii utaelewa maeneo halisi ya mada hii ya leo.
Karibu sana tujifunze pamoja ili tupate Maarifa ya kutusaidia.
Wakati naendelea kusoma vitabu mbalimbali, nilikutana na jambo hili ambalo lilinishangaza kidogo, lakini nilijifunza mambo mengi sana muhimu katika safari ya mafanikio.
Nimeyasoma na kujifunza kutoka kitabu cha KWANINI HADI WEWE SIO TAJIRI kilichoandikwa na Kocha Makirita Amani
Nimeamua nikushirikishe maarifa haya nawe upate kujifunza , na kuchukua hatua ya kuyafanyia kazi.
Mwandishi anaanza kwa kueleza yafuatayo;
Huwezi kufikia utajiri mkubwa na mafanikio kwenye maisha bila ya KUTOA KAFARA.
Mwandishi anaeleza dhana ya TRADE OFF akiwa na maana kwamba " Kupoteza kitu fulani ili kupata kitu kingine , au kuliwa eneo fulani ili uweze kula eneo jingine
Kafara anayozungumzia mwandishi siyo ya kuua watu kwa imani za kishirikina , bali ni kafara ya kukujengea nidhamu itakayokusaidia kufanikiwa sana.
Kafara ya kweli na itakayokusaidia na kukufanikisha kwenye mafanikio makubwa haimuhusishi mtu yeyote , bali inakuhusisha wewe mwenyewe,
Tunazo rasilimali muhimu sana ambazo ni nguvu na muda,
Hapa ninakushirikisha namna ambavyo mwandishi anaeleza kuhusiana na kutoa kafara ,
Na kafara inayozungumza hapa ni ile inayokuhusu wewe , kuacha baadhi ya mambo fulani na kuyafanya mambo fulani ili kuweze kufanikiwa zaidi.
Maeneo matatu muhimu ambayo unapaswa kutoa kafara ili uweze kufanikiwa,
1; VITU UNAVYOFANYA
Kuna vitu vingi unapenda kufanya ambavyo havina mchango wowote kwenye mafanikio unayotaka katika maisha yako.
Hivyo vitu unapaswa kuacha kuvifanya mara moja.
Je, ni namna gani unaweza kuacha?
Mwandishi anaeleza njia na namna sahihi ya kuacha kufanya.
Chukua karatasi na kalamu , Gawa pande mbili
Upande wa kwanza;
Orodhesha vitu vyote ulivyofanya ndani ya wiki 1 , usiache hata kimoja andika vyote ambavyo umevifanya.
Hata kama umetembelea ndugu, umepiga stori na mambo mengine yote usiache hata kimoja.
Upande wa pili;
Orodhesha malengo unayoyafanyia kazi kwenye maisha yako, yaani kule unakotaka kufika.
Orodhesha malengo unayoyafanyia kazi kwenye maisha yako, yaani kule unakotaka kufika.
Pitia upande wa 1 , jiulize kama kinakusaidia kufikia kipi kilichopo upande wa 2 yaani malengo yako.
Kama kina mchango weka alama hii ✅
Kama hakina mchango weka alama hii ❌
Yale uliyoyawekea alama ya ❌ usifanye tena katika maisha yako.
Fanya yale uliyoyawekea alama ya Vema tu(✅)
2.MATUMIZI YAKO YA FEDHA
Kanuni muhimu ni hizi zifuatazo kuhusiana na Fedha;
(1)Matumizi yako kuwa kidogo kuliko kipato na (2) Kuweka akiba na kuwekeza akiba hiyo ili izalishe zaidi.
Kuhusu matumizi yako ya fedha, mwandishi anatufundisha Yafuatayo (Fanya zoezi lifuatalo)
Orodhesha manunuzi yote ambayo umefanya ndani ya mwezi , Baada ya hapo, pitia kila ulichonunua Je, ni kiti cha Muhimu kabisa kwenye maisha yako
Je, maisha yasingeweza kwenda kama usingekuwa nacho?
Kwenye kile ambacho maisha yangeweza kwenda bila ya kuwa nacho , kiwekee ❌ na usikinunue tena.
3.WATU UNAOJIHUSISHA NAO
"Mafanikio yako ni wastani wa mafanikio ya watu watano unaotumia nao muda wako mwingi"
Huwezi kamwe kuvuka nguvu ya watu watano wanaokuzunguka.
Fanya Yafuatayo kuhusiana na jambo hili;
✳️Orodhesha watu wote ambao huwa unatumia muda wako mwingi kuwa nao
Wale unaofanya nao kazi au biashata na wale wanaokuwa nao mara nyingi
✳️Anza kupitia maisha ya kila mmoja ,
Angalia kiwango cha mafanikio ambacho wanacho,
Angalia malengo na mipango waliyo nayo je, ni watu wa kujituma kiasi gani , wenye kiu na mafanikio makubwa au la!
✳️ Waondoe wote wale ambao hawana kiu ya mafanikio makubwa , wakatishao tamaa na walioridhika na pale walipofika.
Hata kama unawapenda kiasi gani unatakiwa kuwaondoa.
Hayo ndiyo maeneo matatu muhimu ambayo unapaswa kutoa kafara ili kuweza kufanikiwa na kufika mbali zaidi
Najua ni maumivu makubwa sana utakayoyapata , lakini kwa kuwa umeamua kufanikiwa huna budi kutoa kafara.
Mwisho;
Mafanikio yoyote yale ni mchakato na wala sio tukio na sio bahati,
Mafanikio yoyote yale ni mchakato na wala sio tukio na sio bahati,
Ni lazima upambane, na ujitoe kikamilifu na yako mambo ambayo utatakiwa uyaacha hata kama ni mazuri kiasi gani,
Kuna watu utatakiwa kuachana nao ili uweze kufanikiwa zaidi, hata kama umetoka nao mbali kiasi gani , kama hawana sifa unazozitaka huna budi kuachana nao.
Sio watu wote utaambatana nao, sio kila aina ya maisha utayaishi, na si kila fashion za nguo na za maisha zitakupitia , zingine lazima uziache ili ufike kule unatamani kufika.
Ahsante sana na Mungu akubariki sana.
#Najifunza kutoka Elimu Kitaa Foundation.
See you Shining and enjoying the cake!;
Wako
Joshua E Golyama
Simu; 0764 257 495
Email; golyamajoshua@gmail.com
Blogu; elimukitaa2020.blogspot.com
Comments
Post a Comment