Skip to main content

MY MEMORIES _MY BRAIN REMEMBER THIS

 MY MEMORIES _MY BRAIN REMEMBER THIS.

Wakati nikiwa mdogo sana, nilijiona nikiwa mwalimu mkubwa sana na mwenye maisha fulani mazuri.

Wakati mwingine nilikuwa na ndoto za kuwa daktari bingwa (Specialization). Ambapo kwa mara ya kwanza nilitamani sana kuwa Daktari aliyebobea kwenye masuala ya kutibu meno.

Nikiwa naanza Kidato cha kwanza, wazo la ualimu liliendelea kuishi ndani yangu hadi kidato cha tatu, ambapo nilibadili wazo hilo na kuanza kufikiri kuwa Mhandishi wa Barabara (Civil Engineering) na nikaanza kuongeza juhudi kabisa katika Hesabu ili niweze kufanya vizuri katika hesabu na kupata nafasi ya kwenda kusomea Mchepuo wa PCM.

Na ninachokumbuka ni kwamba katika mawazo yote hayo niliyokuwa na ndoto nilizokuwa nazo, nilipenda sana kuwaelekeza wengine pale ambapo hawaelewi na wakati mwingine kujipendekeza kuelekeza hata kama sijaombwa kufanya hivyo.

Lakini baadaye kidogo (Mwishoni mwa Kidato cha nne), Nikawaza kuwa Daktari wa Masikio na wazo hili alilirudia mama yangu, baada ya mimi kumuuliza swali "Ety mama unataka niwe Daktari wa nini?" Na Mama yangu akanijibu kuwa anapenda niwe Daktari wa Masikio.

Na Kumbukumbu yangu inaniambia kwamba;Baada ya kuhitimu masomo yangu ya kidato cha nne. Nilianza kutumia simu na kwa mara ya kwanza nilifungua akaunti yangu katika moja ya mtandao wa kijamii (Facebook) na nikafungua pia Ukurasa wa Facebook ulioitwa 'fanatic general' na baadaye  'Ukurasa mwingine ulioitwa "Maneno Ya Ushindi". Katika akaunti hiyo na kurasa zake nilikuwa napenda sana kupakia maandishi yangu huko kila siku na kila wakati nikipata nafasi ya kufanya hivyo. Haijalishi nina cha kuandika au  sina lakini nilihakikisha nimeandikia chochote katika kurasa hizo.........

Nilipata neema ya kufaulu mtihani wangu wa Kidato cha nne na Kujiunga na Kidato cha Tano, mchepuo wa PCB  katika moja ya shule kubwa pale Mkoani Njombe. Huku nikijiona kabisa nikiwa daktari.

Nisingependa kuendelea sana na historia hii Fupi ya Maisha yangu.

Ninachoweza kusema ni kwamba "Hadi muda huu ndoto ya kuwa daktari haipo kabisa ndani yangu" 

Ninachotaka kusema ni Hiki; 

Mwaka 2018 nilipokuwa najiunga na Chuo Kikuu, ndipo nilipoanza kusoma Vitabu. Na Kitabu cha kwanza kukisoma  kilikuwa ni kinaitwa CHANGING YOUR THINKING CHANGING YOUR LIFE kilichoandikwa na Brian Tracy, kItabu hiki kilinibadilisha sana namna ya kuwaza na kuwa na mtazamo tofauti kabisa na vile nilivyokuwa kabla.

Na kitabu cha Pili kilikuwa ni Who am I? Why Am  I here?  cha Sunday Adelaja. Kitabu kilinisaidia sana kujijua mimi ni nani na nimeumba kufanya nini hapa duniani.

Kilinisaidia kujijua ni mambo gani ambayo nayaweza zaidi kuliko mengine.

BAADA YA MAELEZO HAYO MAFUPI , Ninayo mambo Machache Muhimu nataka kukushirikisha leo; 

PENDA NA JENGA TABIA YA KUSOMA VITABU.

Vitabu vinakufungulia dunia vile ilivyo. Inakupa maarifa sahihi.

Ndugu yangu iko watu wengi huishi maisha ambayo hawayafurahii kabisa, na kuona kama hana sababu ya kuendelea kuwepo duniani.

Ziko ndoto nyingi sana ambazo watu walikuwa nazo wakiwa wadogo lakini sasa zimepotea, sababu kubwa Hasa Ni KUKOSA MAARIFA sahihi yenye kuwasaidia Kujua KUSUDI LAO HAPA duniani n namna gani wanaweza kutimiza ndoto zao.

Watu wengi tupo gizani bado, Akili zetu na bongo zetu bado hazijapata nuru (bado hazioni kitu). Hatujajua ni mahali gani ambapo tunaweza kupata Nuru ambayo itatuangazia FIKRA ZETU zilizo gizani bado.

Leo nataka kukushirikisha jambo hili kuwa TUNAWEZA KUPATA MAARIFA kwa Kupitia KUSOMA VITABU. Mambo mengi ambayo huyafahamu utaweza kuyafahamu  hayo baada ya kusoma Vitabu.

VITABU vinatupa UFAHAMU ( kwa yale tusiyoyafahamu bado) na Kisha Kupata MAARIFA kutoka kwenye UFAHAMU na baada ya kutumia MAARIFA tuliyo yapokea na kuyapata kwa usahihi  tunakuwa ni watu wenye hekima.

Hivyo nikuhamasishe zaidi na zaidi uweze kujenga tabia ya kusoma vitabu ili uwezw kufumbuliwa macho.

Changamoto na yale yote unayodhani hayawezi kufanyika, Yanawezekana baada ya KUANZA KUSOMA VITABU kwa kuwa vitakupa mtazamo mpya wa namna ya kuyaendea mambo mbalimbali katika maisha.

Najua umenielewa. Nayawezwekana  hadi muda huu hujajua Kitabu cha Kusoma. 

Nikushauri sasa Kukipata kitabu Hiki Cha SIJAANZA KUISHI kilichoandikwa na Mwanadada Winnie Simplis.

Kwanini SIJAANZA KUISHI. 

Ninakushauri kukisoma kitabu hiki kwa sababu zifuatazo; 

1. Kinatoa na kukupa mwanga wa Kwanini mpaka sasa umeshindwa kumwona yule mtu uliyekuwa unamwon ukiwa mdogo.

2. Kinakusaidia kujua Uwezo wa Kipekee ambao Mungu ameweka ndani yako.

3. Kitakusaidia kujijua na kutambua KUSUDI LA MUNGU katika maisha yako.

4.Kitakuonyesha kama kweli umeanza kuishi au la? 


Inawezekana upo ila bado haujaanza kuishi, Najua nimekuchanganya hapa na pengine kushindwa Kuelewa. Ukikisoma kitabu hiki kitakusaidia kujibu maswali hayo ambayo unajiuliza. Mimi sikuyajua kabla. Ila baada ya kusoma Kitabu kile nimeweza kujua kama ninaishi au bado Sijaanza.


Bila shaka umepata shauku ya kuanza kusoma vitabu sasa. Wasiliana na mimi ili nikupe maelekezo ya namna ya kuchagua vitabu vya kusoma  na Namna ya kuvisoma.


Pia, Kama unahitaji Kupata Nakala Yako ya Kitabu hiki cha SIJAANZA KUISHI. Wasiliana nami  nikupe maelekezo ya Kukipata nakala  yako.

Au tumia mawasiliano yaliyopo hapa chini kwenye Picha ili nakala yako kwa mkoa wowote uliopo hapa TANZANIA.


Sijaanza Kuishi Na Winnie Simplis.


See You Shining And Enjoying The Cake! 

Joshua Golyama 

(Author | Motivational Speaker | Teacher | Blogget).

+255 764 257 495 (Whatsapp).

golyamajoshua@gmail.com

elimukitaa2020.blogspot.com


"I se The Whole World Enjoying Because Of Me"

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUANZA UPYA

  Kuanza upya ni jambo zuri ambalo linawezekana katika maeneo mengi ya maisha yetu, iwe ni kazi, uhusiano, au malengo binafsi. Hapa kuna hatua kadhaa unazoweza kuchukua kuanza upya: 1. Tathmini hali ya sasa Anza kwa kufanya tathmini ya hali yako ya sasa.  Jiulize maswali kuhusu maeneo gani unataka kuboresha au kubadilisha. Je, kuna mambo yanayokukwamisha au kukuzuia kufikia malengo yako? Kuelewa hali yako ya sasa ni hatua muhimu katika kuanza upya. 2. Weka malengo Weka malengo wazi na sahihi. Fikiria kwa kina kile unachotaka kufikia na kuamua hatua za kuifikia.  Malengo yako yanapaswa kuwa ya kusisimua, lakini pia yapaswa kuwa ya kufikika na yanayopimika.  Andika malengo yako na uwaeleze kwa uwazi. 3. Panga mpango wa utekelezaji Panga mpango wa vitendo wa jinsi utakavyotekeleza malengo yako. Tambua hatua ndogo na za kivitendo unazoweza kuchukua ili kufikia malengo yako.  Kwa kila hatua, weka muda uliopangwa na rasilimali zinazohitajika. 4. Jifunze kutokana na uz...

AGRICULTURE 101; KILIMO CHA TEMBELE

Habari   rafiki   mpendwa , Karibu   sana   katika   Makala   hii   Ya   Kilimo   na   Ufugaji Na   leo   tunakwenda   kuangalia   kuhusiana   na   Kilimo   Cha   Tembele. Mboga   nzuri   sana   na   inayopenda   na  kutumiwa   na    watu   wengi   sana   duniani Makala   hii   itakuwa   na   Sehemu/Vipengele   vifuatavyo; 1.Utangulizi 2.Aina za Tembele 3.Faida za Kiafya zitokanazo na Tembele 4.Namna Ya Kuandaaa Shamba 5.Kupanda 6 Kuvuna Karibu     sana    tujifunze   kuhusu    tembele. Kilimo cha tembele Kitaalamu    tembele   hujulikana   kama  ...

KARIBU KATIKA PROGRAM YA ELIMU KITAA(LEARNING SITE)

  Elimu Kitaa Foundation inakukakaribisha Katika Program ya Elimu Kitaa Habari ya kwako rafiki yangu. Bila shaka uko vizuri na unaendelea vyema na majukumu ya kila siku. Naitwa Joshua Golyama  mwanafunzi wa Shahada ya awali ya Sayansi ya Kilimo kwa Ujumla(Bsc.Agriculture General) kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine Cha Kilimo (SUA                                         Mwanzilishi wa Program inayoitwa ELIMU KITAA. Leo ninapenda kukuletea maeneo mbalimbali ambayo unaweza yatembelea na tukajifunza pamoja na mimi. Maeneo hayo utapata nafasi ya kusoma makala ambazo ninaziandika kila siku na kuziweka humo, na tukajifunza kwa pamoja na kupata maarifa zaidi na zaidi. Kwanza kabisa nikupe utangulizi wa maana halisi ya Neno hili ELIMU KITAA. Elimu Kitaa ni program inayohusika na kuandika makala mbalimbali katika mitandao ya Kijamii na kuandaa semina mbalimbali zenye kutupa maarifa muhimu san...