Skip to main content

AFYA; FAHAMU KUHUSU PARACHICHI NA UMUHIMU WAKE MWILINI

FAHAMU KUHUSU PARACHICHI NA UMUHIMU WAKE MWILINI 


Habari yako  mpendwa,

Ni matumaini yangu kwamba u mzima na waendelea vyema na maisha ya kila siku, huku ukitafuta na kunia kufikia mafanikio makubwa sana maishani mwako.
Karibu sana tuweze kujifunza kuhusu Afya, na leo tunaangalia tunda linaloitwa  parachichi pamoja na umuhimu katika mwili wa Mwanadamu.
Miongoni mwa vyakula vinavyohitajika ili kukamilisha mlo kamili ni MATUNDA, matunda hutupatia faida nyingi sana katika miili yetu .Yapo matunda mengi sana na yote yana faida kubwa sana katika Mwili wa  Mwanadam.

Leo tunakwenda kufahamu kiundani kuhusu Parachichi na faida zake katika Mwili wa Mwanadamu.

Karibu sana ndugu yangu tujifunze na tuanze kulitumia tunda hili baada ya kujua faida nyingi tuzipatazo wakati tunatumia tunda hili
   Parachichi (avocado) Persea americana

Tunda aina ya parachichi hujulikana kama embefuta kwa sababu limejaa mafuta yenye faida nyingi sana katika afya ya mwanadamu 

Tunda hili husifika sana kwa sababu lina virutubisho vyingi sana ambavyo vina umuhimu mkubwa katika mwili wa binadamu.

Chimbuko la Parachichi Kusini-Kati Mexico na America Ya Kati, miaka ya 7000 na 5000 B.C( Kabla Ya Kristo).

Parachichi ni tunda la kipekee sana .Vitabu vingi na tafiti nyingi zinaonyesha kuwa parachichi ni tunda lenye manufaa makubwa sana kiafya.

Virutubisho(nutrients) vinavyopatikana kwenye tunda aina ya parachichi.
Kutoka kipande kimoja cha parachichi(100 gram) kinatupa virutubisho hivi vifuatavyo; 

Vitamini B-5        28%                       Copper  21%
Vtamini B-6  15%                              Folate  20% 
Vitamini K    18%                              Vitamini  B-6    15%
Vitamini B-2(Riboflavin) 10%          Vitamini E  14% 
Vitamini B-3(Niacin) 11%                 Potasium  10%
Magnesium 7%                                  Manganese 6%
Vtamini B -1(Thiamine)   6%            Zinc        6%
Chlorine    3%                                    Vitamin D    -
Vitamin B -12   --                              Vitamini C   11%

 Folate  Husaidia seli za Mwili kufanya kazi vile inavyotakiwa (normal function) , na Asidi hii ya Folate  muhimu sana kwa Mama mwenye mimba .

Lutein na Zeazonthin -Husaidia katika afya ya macho matatizo ya macho yanayotokana na umri.Husaidia na kuzuia jicho(macho) -seli na tishu za macho kutokuharibiwa na mwanga wa jua. Husafisha  miale hatari ya mwanga na kuhakikisha selli za macho zinakuwa salama 
Tafiti zinaonyesha pia kuwa endapo Karetonoid(Caretonoides) Yaani Luetin na Zeazonthin zikiwa za kutosha katika seli za jicho husaidia kuona  vizuri.

Hizo ni baadhi ya virutubisho tunavyovipata kwa kula Parachichi. Lengo kubwa la Makal hii ni kukufahamisha kuhusu umuhimu wa parachichi  katika afya yako. Baada ya kusoma makala hii, hakikisha unajitahidi kuongeza tunda hili la parachichi katika mlo wako ili usikose virutubisho vyingi sana na vya muhimu sana kwa afya yako.

FAIDA ZA KIAFYA ZITOKANAZO NA  KULA PARACHICHI; 

1.Parachichi ina virutubisho vitatu muhimu ambavyo miili yetu  inategemea Wanga ,  Protein na Mafuta. Hivi virutubisho ni muhimu sana kwa afya ya binadamu kwani husaidia kuongeza nguvu za mwili , na kinga ya mwili pia.

2.Huboresha afya ya Ubongo(Healthy brain)
Katika parachichi tunapata madini ya Kopa(Copper)  inayohusika na uzalishaji  wa Myelin na kuhakikisha upatikanaji wake, husaidia  katika Upokeaji na kutafsiriwa kwa taarifa kutoka vichocheo vya nje.

3.Hukuweka katika hali nzuri (mood ) nzuri.
Tafiti zinaonyesha kuwa watu wenye msongo wa mawazo wana upungufu mkubwa wa madini ya Kalsiam. Hivyo kutumia parachichi katika mlo wako kunaweza kusaidia kukuweka katika mood nzuri 

4.Ni muhimu sana kwa Wamama wajawazito.
 Kwa kuwa parachichi lina asidi ya Folate , Potasiam,  Vitamini C na Vitaminj B-6 ambazo ni muhimu na  husaidia afya na Ukuaji wa mtoto tumboni. Pia husaidia kupunguza hatari ya kuharibika kwa mimba changa.

5.Hupunguza hatari ya kupata magonjwa kama vile Unene uliopitiliza, Kisukari na magonjwa .
Tafiti mbalimbali zinaonyesha kuwa kula mlo wenye mchanganyiko (mjumuisho ) wa matunda kama vile parachichi hupunguza hatari ya kupata magonjwa ya moyo, kisukari na unene uliopitiliza(Obesity)

6.Parachichi ina mafuta mengi  sana (fat ) lakini ni mafuta mazuri ambayo yanaitwa kwa Kiingereza "Mono unsaturated fats"  ambayo ndiyo mafuta mafuta yanashauriwa kutumika katika chakula.
Aina hii ya mafuta husaidia katika afya ya moyo.

7.Parachichi husaidia umeng'enyaji wa chakula kufanyika vizuri(metabolic process).Mchakato wa kuvunja-vunja , virutubisho vilivyofonzwa na mwili ili kuweza kuzalisha nishati itakayotumika katika shughuli za mwili za kila siku.

8.Parachichi ina kiwango kikubwa sana cha Mafuta , ambayo ni "monounsaturated fats"  ambayo ni mafuta mazuri-Husaidia kupunguza kiwango cha Cholestrol (lehemu )mwilini 
Lehemu(cholestrol) ina madhara makubwa saba katika afya ya binadamu , kama itakuwa  katika kiwango kikubwa. lakini pia cholestrol ina umuhimu mkubwa sana katika mwili wa binadamu kama itakuwa  katika kiwango kinachotakiwa.

9.Parachichi inasaidia kusawazisha kiwango cha madini ya Sodiam kwenye miili yetu .Kuzidi kwa kiwango cha sodiam mwilini huongeza shinikizo la damu, pia huongeza hatari ya kufeli kwa moyo , kansa ya tumbo (stomach cancer) magonjwa ya figo na kiharusi .
10.Huzuia saratani .Hupunguza kasi ya ukuaji wa selu za saratani ya tezi dume.



Hadi hapo tumeweza kufahamu kwa uchache kuhusiana na Parachichi, virutubisho vinavyopatikana  kwenye  parachichi, na faida zake tuzipatazo.Kwa kuyajua haya tuna kila sababu ya kutumia tunda hili kwa wingi  sana kutokana na umuhimu ambao tumeweza kuupata kupitia Makala hii 

Ubarikiwe sana kwa Kujifunza hayaa.Yachukue na Anza kuyatendea kazi.


______________________________________________________________________________________________
Makala hii imeandikwa na ; 
Joshua Golyama 
Mwanafunzi wa Shahada Ya Awali Ya Sayansi Ya Kilimo 
Chuo Kiikuu Cha Sokoine Cha Kilimo (SUA-MOROGORO)
+255764257495
Barua pepe; golyamajoshua@gmail.com
Blogu ; elimukitaa2020.blogspot.com






Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUANZA UPYA

  Kuanza upya ni jambo zuri ambalo linawezekana katika maeneo mengi ya maisha yetu, iwe ni kazi, uhusiano, au malengo binafsi. Hapa kuna hatua kadhaa unazoweza kuchukua kuanza upya: 1. Tathmini hali ya sasa Anza kwa kufanya tathmini ya hali yako ya sasa.  Jiulize maswali kuhusu maeneo gani unataka kuboresha au kubadilisha. Je, kuna mambo yanayokukwamisha au kukuzuia kufikia malengo yako? Kuelewa hali yako ya sasa ni hatua muhimu katika kuanza upya. 2. Weka malengo Weka malengo wazi na sahihi. Fikiria kwa kina kile unachotaka kufikia na kuamua hatua za kuifikia.  Malengo yako yanapaswa kuwa ya kusisimua, lakini pia yapaswa kuwa ya kufikika na yanayopimika.  Andika malengo yako na uwaeleze kwa uwazi. 3. Panga mpango wa utekelezaji Panga mpango wa vitendo wa jinsi utakavyotekeleza malengo yako. Tambua hatua ndogo na za kivitendo unazoweza kuchukua ili kufikia malengo yako.  Kwa kila hatua, weka muda uliopangwa na rasilimali zinazohitajika. 4. Jifunze kutokana na uz...

AGRICULTURE 101; KILIMO CHA TEMBELE

Habari   rafiki   mpendwa , Karibu   sana   katika   Makala   hii   Ya   Kilimo   na   Ufugaji Na   leo   tunakwenda   kuangalia   kuhusiana   na   Kilimo   Cha   Tembele. Mboga   nzuri   sana   na   inayopenda   na  kutumiwa   na    watu   wengi   sana   duniani Makala   hii   itakuwa   na   Sehemu/Vipengele   vifuatavyo; 1.Utangulizi 2.Aina za Tembele 3.Faida za Kiafya zitokanazo na Tembele 4.Namna Ya Kuandaaa Shamba 5.Kupanda 6 Kuvuna Karibu     sana    tujifunze   kuhusu    tembele. Kilimo cha tembele Kitaalamu    tembele   hujulikana   kama  ...

KARIBU KATIKA PROGRAM YA ELIMU KITAA(LEARNING SITE)

  Elimu Kitaa Foundation inakukakaribisha Katika Program ya Elimu Kitaa Habari ya kwako rafiki yangu. Bila shaka uko vizuri na unaendelea vyema na majukumu ya kila siku. Naitwa Joshua Golyama  mwanafunzi wa Shahada ya awali ya Sayansi ya Kilimo kwa Ujumla(Bsc.Agriculture General) kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine Cha Kilimo (SUA                                         Mwanzilishi wa Program inayoitwa ELIMU KITAA. Leo ninapenda kukuletea maeneo mbalimbali ambayo unaweza yatembelea na tukajifunza pamoja na mimi. Maeneo hayo utapata nafasi ya kusoma makala ambazo ninaziandika kila siku na kuziweka humo, na tukajifunza kwa pamoja na kupata maarifa zaidi na zaidi. Kwanza kabisa nikupe utangulizi wa maana halisi ya Neno hili ELIMU KITAA. Elimu Kitaa ni program inayohusika na kuandika makala mbalimbali katika mitandao ya Kijamii na kuandaa semina mbalimbali zenye kutupa maarifa muhimu san...