George Bernard Shaw aliwahi kusema maneno haya......"beware of false knowledge, it is more dangerous than ignorance"
Kwamba "Kuwa makini sana na taarifa zisizo sahihi, kwa sababu ni hatari zaidi kuliko ujinga"
Taarifa ni kitu cha msingi sana, unapohitaji kufanya jambo fulani.
Ukweli ni kuwa unahitajika kuwa na taarifa nyingi, kabla ya kufanya jambo.
Lakini taarifa hizo lazima ziwe sahihi sana, kwa sababu zisipokuwa sahihi zitakupelekea mahali pabaya.
Ili ufanye vyema katika jambo fulani, unalazimika kuwa na taarifa nyingi na zilizo sahihi.
Kuwa makini sana na vyanzo vya taarifa yako
Fanyia tathmini kwanza, juu ya chanzo cha taarifa, Je, ni sahihi na zitakufaa.
Kumbuka, Maamuzi yoyote yale yanategemea taarifa ulizo nazo.
Kufeli au kufanikiwa kunategemea na taarifa ulizo nazo.
Kiwango cha usahihi wa taarifa huamua aina ya matokeo ambao unakwenda kuyapata.
..Wito wangu ni kuwa, tuko katika karne ya TAARIFA, karne ambayo walio na taarifa sahihi ndio wanaofanikiwa.
Na kumbuka pia, Karne hii kuna mafuriko makubwa sana ya taarifa, kila mmoja anatoa taarifa zake anazozijua.
Hivyo, usipokuwa makini unaweza kupotezwa kabisa.
Hakikisha unatathmini usahihi wa taarifa kabla ya kuzifanyia maamuzi.
NB: Hii inafanya kazi maeneo yote ya Maisha, Hadi kwenye Ndoa kule, Usifanye maamuzi kama hauna taarifa sahihi.
Usisambaze taarifa ambayo hauna uhakika kama ni sahihi.
....... kumbuka Taarifa isiyo sahihi ni BOMU ambalo laweza kukulipua na kukuua kabisa.
Neno la Mungu kiwe ni chanzo cha kwanza kabisa cha taarifa zako zote, na vyanzo vingine vitafuata.
©Elimu Kitaa Foundation
Comments
Post a Comment