Kila jambo unalolifanya, lifanye kama wajibu, na usifanye ukitegemea kutambuliwa, au kupewa shukrani.
Watu wengi wanapata shida sana pale ambapo wanafanya mambo mengi, na hakuna anayeonekana kuwashukuru kwa yale wanayoyafanya.
Unajitoa kwa nguvu zako kuhakikisha kila kitu kinakuwa sawa.
Fuatilia mifano hii michache ili uweze kupata kile ninachokimaanisha hapa;
Mfano wa kwanza; Viongozi mbalimbali tulio nao, wanatumia muda wao mwingi na nguvu nyingi kuhakikisha wale wanaowaongoza wanafika pale wanapotakiwa kuwa.
Na hakuna hata mmoja anayetambua mchango wao na nguvu zao walizotumia kuwaongoza.
Na pengine asiwepo hata mmoja wa kusema asante kwa yale wanayafanya.
Mfano wa Pili; kwenye mahusiano,unakuta boyfriend/girlfriend anafanya kila anachoweza ili kuboresha mahusiano yao, kumsaidia kwa kila hali/changamoto anayoipitia Lakini haoni mwenzie akimshukuru au kutambua kwa kile anakifanya.
Mfano wa tatu; Kazini kwako, unafanya kila kitu vile inavyotakiwa, labda kila siku unawahi kufika kazini na hakuna anayetambua mchango wako hapo kazini kwako.
Na pengine unaweza ukawa umefanya jambo kwa nguvu zako zote halafu anayekuja kutambuliwa kwa kukamilika jambo lile ni mtu mwingine tofauti na wewe uliyehusika.
Mfano wa nne; Wazazi wetu pia wanatumia nguvu nyingi sana na muda wao mwingi, mali zao na kila kitu kuhakikisha watoto wao wanasoma na kufikia maisha mazuri.
Lakini cha kushangaza, hakuna mtoto anayetambua ule mchango mkubwa ambao wazazi wamefanya kwa watoto wao.
Mfano wa Mwisho; Unatuma jumbe kwa mtu fulani au, unampigia simu kila siku au kila wakati, lakini hutaona yeye amekutumia Ujumbe wowote au kukupigia simu.
Wewe unamtafuta kila siku na kila wakati , lakini yeye hana muda wa kukutafuta kabisa.
Kwa mifano hiyo hapo juu, bila shaka inaweza kuwa changamoto kwako na pengine kushindwa kuendelea kumtafuta au kufanya kile ulichokuwa unakifanya.
Na kama utakifanya ,basi utakifanya kwa nguvu ndogo na si katika ubora ule wa mwanzo.
Na usipojua nini cha kufanya, unaweza kuharibu kabisa mwelekeo wako na vile ambavyo hapo kabula ulikuwa unafanya.
Ili usiumie na kupata shida kwa yale ambapo huoni mtu anatambua kile unakifanya unatumia nguvu nyingi na muda mwingi lakini hakuna anayekuja kukushukuru au hata kusema ahsantee.
Yafahamu yafuatayo na kisha anza kuyafanyia kazi;
*️⃣ Usifanye jambo ili mtu fulani akutambue au mtu fulani aje kukushukuru.
*️⃣ Jua kuwa kile unachokifanya ni wajibu wako, hivyo fanya ukijua kuwa ni wajibu wako.
*️⃣Sio wote wanaweza kutambua kile unachokifanya, lakini upo wakati watatambua kile ulichokuwa unakifanya.
Pengine utakuwa haupo mahali hapo ndipo watakapotambua umuhimu wako.
*️⃣Kufanya jambo ili utambuliwe na kupewa shukrani kuna athari kubwa zaidi, ikiwemo kupunguza nguvu ya kukifanya kile kitu, na kushindwa kufikia malengo yako uliyoyakusudia.
Yajue haya ili yaweze kukusaidia na kujua kuwa unatakiwa kufanya kama wajibu wako na sio kufanya ili utambuliwe na mtu fulani.
Mungu akubariki sana.
#Hekima Ya Siku.
ELIMU KITAA.
_____________________________________________________
Makala hii imeandikwa na;
Joshua Golyama
golyamajoshua@gmail.com
+255 764 257 495
elimukitaa2020.blogspot.com
Comments
Post a Comment