MAKALA 01; RAFIKI BORA NI VITABU (THE BEST FRIEND IS BOOKS)
Habari yako rafiki yangu, Ni matumaini yangu kwamba u mzima wa afya kabisa,
Karibu katika mfulululizo wa makala hizi kutoka katika kitengo cha KUTOKA VITABUNI,
Ili kuweza kuwa
bora katika maisha yako ni vyema sana ukaambatana na kuzungukwa na watu walio
na kile ambacho wewe unataka kuwa. Ni asilimia 85% ya mafanikio yako huchangiwa
na watu wanaokuzunguka.
Marafiki zako, ndugu zako na jamaa zako ambao unatumia muda mwingi kuwa nao kazini, shuleni, ofisini na maeneo mbalimbali ni muhimu wakachunguzwa na kuona kama wanaweza kukupeleka kule ambako unataka kufika.
Upo msemo wa Kiswahili ambao huzungumzwa kwamba ukitembea na mwizi na wewe utakuwa mwizi, hii humaanisha kwamba ukiambatana na mtu mwenye tabia Fulani,automatically kuna baadhi ya mambo ambayo utayavuta kutoka kwa rafiki yako.
Eneo hili ni muhimu sana kwa sababu linachangia kwa kiwango kikubwa katika mafanikio yetu na katika safari ya kufika kule ambako tunatamani kufika.
Neno la Mungu
linadhibitisha hili; Tuangalie mifano michache hapa;
Mithali 13:20 “Enenda pamoja na wenye hekima, nawe utakuwa na hekima. Bali rafiki wa wapumbavu ataumia”
Mithali 22:24-25 “Usifanye urafiki na mtu mwenye hasira nyingi; wala usiende na mtu wa ghadhabu nyingi;
Usije ukajifunza njia zake; na kujipatia nafsi yako mtego.
Mithalio 27:19 “Kama uso ufananavyo na uso katika maji; Kadhalika moyo wa mtu na mwenzake”
Mithali 27:17 “Chuma hunoa chuma; Ndivyo mtu auonoavyo uso wa rafiki yake”
Kutoka kwenye
mifano michache ambayo tumeiona hapo juu tunajifunza mambo ambayo hutokea pale
tunapokuwa tunaambatana na wale marafiki zetu, familia na wengine na matokeo
yake.
Mfalme Sulemani
anatufundisha hapa kwamba Kamwe usifanye urafiki na mtu mwenye hasira kwa sababu unaweza
kujifunza pia na wewe.
Unapokuwa unatumia muda wako mwingi na rafiki yako, kuna kuambukizana tabia kunatokea. Hivyo kuna baadhi ya mambo mtaanza kufanana katika mitazamo na hata utendaji wake.
Tunajifunza pia
kwamba ili kuwa mtu mwenye hekima ni lazima uambatane na wenye hekima, utumie
muda wako mwingi na watu wa aina hiyo.
Najua unayo ndoto ambayo unatamani kuitimiza katika maisha yako, jambo la muhimu sana ambalo unatakiwa kuwa nalo makini ni AINA YA MARAFIKI utakaoambatana nao. Bila shaka utapaswa kuwa makini hasa kuchunguza mitazamo waliyo nayo, na hata ndoto zao, misimamo yao na kuona kama inafanana na wewe na kukusaidia kukuvusha sehemu moja kwenda nyingine katika safari ya mafanikio yako.
Moja ya marafiki ambao unaweza kuwachagua kuambatana nao na ukatumia muda wako mwingi ni VITABU. Najua unashangaa hapa kidogo lakini ambatana na mimi katika kusoma makala hii utajifunza na kujua hasa kwanini kuambatana na VITABU.
Waliotutangulia walijihusisha katika mambo mengi sana, kuna mahali walifana vizuri sana, kuna mahali walifanya vibaya na hayo yote wameyandika kwenye VITABU. Naweza kusema kuwa Kitabu ni moja ya hazina kubwa sana ambayo wazee wetu wa zamani walituachia, na hata sisi tunawaachia na tutawaachia yale tunayoendelea kujifunza kila siku.
Kwenye vitabu kuna kila kitu ambacho wewe unakihitaji ili kufikia ndoto zako kwa mafanikio makubwa sana. Unapata kuhamasika na yale ambayo yalifanyika hapo zamani yanayofanana na lile ambalo wewe unalifanya.
In the books you extract the positive mindset that is needed in accomplishing your dreams/purpose and enables you to live victorious life.
Unatakiwa kuambatana na Yule ambaye haamini katika kushindwa na badala yake anaamini katika kushinda. Mwenye anaona sababu lukuki za kulifanikisha lile ambalo unataka kulifanya. Naye si mwingine bali ni VITABU.
Wako marafiki wengine ambao wana mitazamo hasi, wanaamini katika kushindwa na pengine kuwa na sababu na visingizio vingi vya kutofanya au kuendelea na kile wanachokifanya.
Wanaopenda
Kukata TAMAA kila wakati, Wasiotaka kujifunza kila siku, wasiotaka kukosolewa
na mengine mengi.
HAWAKUFAI WATU
WA AINA HII, na una kila sababu ya kuwaacha na kuchagua marafiki wengine wazuri
wanaoweza kukusaidia, kukufundisha, kukuelekeza njia sahihi ya kufika kule
ambako wewe unataka kufika.
Bila shaka Rafiki KITABU ndiye rafiki bora sana na ambaye kila mmoja wetu anapaswa kuomba Urafiki naye na kasha kuambatana naye kwa kila hatua ambayo tunazipiga kila siku.
Na sio KITABU tu bali KITABU SAHIHI, huyu atakusaidia sana kufika kule unakotaka kufika, huyu anakuletea story za watu mbalimbali waliotangulia ambao walifanya mambo mbalimbali, wengine walishindwa na wengine walifanikiwa sana.
Rafiki huyu atakusimulia story ya wale ambao hawakuona sababu hata moja ya kukata tamaa licha ya changamoto mbalimbali ambazo walikabiliana nazo, mfano Kukosa PESA, KUKATALIWA, ULEMAVU na zinginezo nyingi ambazo wewe unazifahamu au kuzisikia.
Bila shaka kwa kusimulia story hizi za kweli zitakuhamaisha wewe na pengine kukupa nguvu zaida kusonga mbele bila ya kukata tamaa.
Na rafiki huyu anayo orodha ya watu wengi ambao waliwahi kufanya kile ambacho wewe unatamani kukifanya, kwa kupitia kuwafahamu watu hawa utajifunza njia ambazo wao walizitumia, changamoto na mafanikio makubwa sana ambayo waliyapata.
Na utajua ni wapi pa kuanzia safari yako, milima na mabonde na namna utakavyoweza kukabiliana nayo.
Lakini rafiki huyu KITABU atakuunganisha na watu wengine wakubwa na wenye Hekima na Busara katika kufanya mambo mablimbali. Waflame, Wafanya biashara wakubwa, Bilionea na watu wenye sifa mbalimbali hapa duniani.
Anakufungulia dunia nzima na kuileta mahali ulipo, unapata nafasi ya kuyafahamu mambo mbalimbali kwa upana wake.
Bila shaka hautajuta
kabisa kuwa naye maishani mwako.
This is my best friend ever to have on earth, because teaches me and direct me in the right way.
Huyu ndiye rafiki ambaye mimi rafiki yako nakuletea kwako hivi leo, tafadhali fanya urafiki naye, na kamwe hautajua kabisa kumfahamu.
MUHIMU; Ambatana nasi katika mtaa wetu ambako rafiki huyu ninayekusimulia
habari zake kila siku anapatikana, na huku tunapiga naye story na hakika
anatufundisha mambo mengi sana ambayo yanatufaa katika maisha yetu ya kila
siku, na kutupatia UFAHAMU, MAARIFA NA UFAHAMU.
Mtaa huo unaitwa
Street of Books (Mtaa wa Vitabu) huku tunayo mada moja tu ya KUJIFUNZA NA
KUSOMA VITABU.
Karibu sana
katika mtaa huu kwa sababu ni mtaa bora sana kuwahi kuwahi kuwepo.
Kujiunga na sisi
tembelea mtandao wa Instagram kwa jina hili @streetofbooks_ na utakuwa miongoni
wa wana mtaa huu.
Ahsanteni sana
na Mungu akubariki sana kwa kujifunza name katika makala hii. Usikose kutufuatilia katika ukurasa wetu wa
Instagram wa @streetofbooks_ kila siku ili kujifunza zaidi na kupata hamasa ya
kusoma vitabu na kupata maarifa yaliyomo humo.
Makala hii
imeandikwa na;
Joshua Golyama
(Mwandishi,
Mwalimu, Blogger na Mwazilishi wa Taasisi ya Elimu Kitaa Foundation).
Mawasiliano; +255 764 257 495/.
Comments
Post a Comment