ANZA SASA KUFANYA, UMRI ISIWE KIKWAZO KWAKO.
Bila shaka unayo maono fulani (Unajiona ukiwa unafanya kitu baadaye ambacho ni kikubwa sana). Kwa namna fulani unatambua jambo fulani unaweza kulifanya kwa ufanisi mkubwa kabisa.
Na unajua kabisa, kwamba utakapofanya jambo lile utakuwa katika viwango fulani vikubwa sana.
Lakini, mbona huanzi? Nini kinakukwamisha usiendelee?
Ni ujuzi, Maarifa, huelewi pa kuanzia? Au unasema ngoja nikue kidogo au nifikie hatua fulani?.
Tuko watu ambao tunasubiri hadi tufike viwango fulani vya Elimu ndipo tuanze kutumiza ndoto zetu.
Tuko watu tunaosubiri tufikie Umri fulani ili tuanze kutimiza ndoto zetu.
Lakini tunajichelewesha wenyewe, umri sio tatizo kabisa.
Kwani haujaona Watu wakiwa na Umri mdogo na wanafanya Makubwa?.
Je, Mastaa wengi katika tasnina mbalimbali duniani wana Miaka mingapi hadi muda huu na walianza wakiwa na Miaka mingapi?
Je, Mabilionea wa Dunia wana Miaka mingapi muda huu?.
Je unamfahamu Rev Victor Githu kutoka Kenya ambaye alianza kuhubiri akiwa na Miaka Mitano (5) na sasa anafanya vizuri sana.
Je, Wewe una miaka mingapi hadi muda huu? Na bado unasema wacha nikue kue.
Je, Haujasoma Biblia; Wafalme walianza Kutawala wakiwa na Miaka mingapi?
Ngoja Nikuonyeshe kidogo hapa.
Manase alianza Ufalme akiwa na Miaka 12 (2 Nyakati 33:1)
Yoashi alianza kutawala akiwa na Miaka 7.(2 Nyakati 24:1).
Yosia alianza akiwa na Miaka 12 ( 2 Nyakati 34:1)
Na wafalme wengi waliotawala Taifa la Israel walianza wakiwa na Miaka 20-25, Wakiwa bado wadogo kabisa.
Na iko mifano mingi sana na Ya watu ambao wameanza Kutumiza Malengo na ndoto zao wakiwa wadogo kabisa (Vijana).
Nini kinachokuzuia wewe kutoanza.
Jiamini wewe mwenyewe (Believe on yourself that you can do great things according to the vision you have)
Unakumbuka Mungu alimwambia nini Yeremia wakati anajitetea kwamba Yeye ni mtoto mdogo.
Yeremia 1 (SUV)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
⁷ Lakini Bwana akaniambia, _Usiseme, Mimi ni mtoto; maana utakwenda kwa kila mtu nitakayekutuma kwake, nawe utasema kila neno nitakalokuamuru._
⁸ _Usiogope kwa sababu ya hao maana mimi nipo pamoja nawe nikuokoe, asema Bwana._.
Hadi hapo sasa, naona umeshaacha kujitetea ety kwa sababu ya Umri.
Hakuna sababu inayoweza kukuzuia wewe kutotimiza ndoto zako. Jiamini na anza kuchukua hatua sasa.
Usitake kuanzia pa kubwa, anza kidogo kidogo kwa Uaminifu mkubwa na Uvumilivu mkubwa na Kujitoa bila shaka utaushangaza ulimwengu kwa kutimiza ndoto zako
Kumbuka; Kutotimiza ndoto zako ni kuwanyima haki wale ambao wangefaidika na kutimizwa kwa ndoto zako.
Anza sasa, Umri ni namba kwa kuwa UPO UWEZO MKUBWA NA WA KIPEKEE ambao umewekwa ndani yako.
See You Shining And Enjoying The Cake!!
Joshua Golyama
+255 764 257 495
elimukitaa2020.blogspot.com
Elimu Kitaa Foundation
Comments
Post a Comment