Skip to main content

JENGA TABIA YA KUJIFUNZA KILA WAKATI , ONDOA KIBURI KATIKA KUJIFUNZA.


JENGA TABIA YA KUJIFUNZA KILA WAKATI ,  ONDOA KIBURI KATIKA KUJIFUNZA.

Unapokosa tabia ya kujifunza na kuwa na hali ya kujiona unajua kila kitu utakuwa nayo na Kwa Maana Hiyo hautaweza kuwa na spirit ya kuendelea kujifunza zaidi na zaidi.

Lakini unapokuwa unajifunza kila wakati, utagundua kwamba Mambo mengi huyajui hii itaamusha Nguvu mpya, ari mpya na hamasa ya kue ndelea kujifunza zaidi.

Jifunze zaidi ili upate hamasa ya kujifunza zaidi.
Na MUHIMU,  ili uweze kujifunza ni lazima ujione hujui , na kama utaona kama unajua kamwe hautaweza kujifunza

Kwa maneno Mengine unakuwa na KIBURI KATIKA KUJIFUNZA ambacho Kinakuzuia wewe kujifunza zaidi, kwa sababu ndani yako kutakuwa na Sauti kama hii  'mbona kila kitu ninakijua, kujifunza ni kupoteza muda'

Hakikisha unajitahidi unakuwa na Tabia Ya KUJIFUNZA, kwa sababu katika Karne hii Ya 21 kuna Maendeleo makubwa sana Ya Teknolojia na Ni ULIMWENGU WA TAARIFA hivyo usipojifunza kamwe hauwezi kuwa na Taarifa sahihi za kukusaidia kuendana na kasi ya Maisha ya Ulimwengu wa sasa.

Zipo njia nyingi ambazo unaweza kujifunza

MOJA; Kwa kusoma Vitabu, kitu ambacho hujajua ni kwamba katika vitabu kuna Hazina kubwa sana, ambayo ni msaada sana kwako.
Kitu ambacho wewe hukifahamu , wapo wanaokifahamu na Wameandika kwenye Vitabu.
Hivyo, Anza kusoma vitabu ili uweze kuipata hazina ambayo imefichwa kwenye vitabu.

MBILI; Kupitia Changamoto unayoipitia au Changamoto ambayo watu wengine wanaipitia.
Kila changamoto inayotokea katika maisha yako ina darasa ndani yake, kuna kitu cha kujifunza
Tatizo ni kwamba watu wengi wanapopata changamoto, wanaitazama kwa upande mmoja na Si katika pande mbili, 

Katika changamoto kuna Fursa ya kujifunza, na kuweza kubadili ufanyaji wa mambo na kazi yako.
Pia, changamoto ambazo watu wengine wanazipitia tunayo nafasi pia ya kujifunza kwa namna ambavyo wanakabiliana na changamoto wanazozipitia.

Bila shaka umepata kitu tayari kwa siku ya leo.
Jenga tabia Ya Kujifunza kila wakati na Kila siku.

See you shining and enjoying the cake!

Makala hii imeandikwa na; 
Joshua Golyama (Mhamasishaji Na Mwandishi)
Whatsap number  0764 257495
Email; golyamajoshua@gmail.com


Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUANZA UPYA

  Kuanza upya ni jambo zuri ambalo linawezekana katika maeneo mengi ya maisha yetu, iwe ni kazi, uhusiano, au malengo binafsi. Hapa kuna hatua kadhaa unazoweza kuchukua kuanza upya: 1. Tathmini hali ya sasa Anza kwa kufanya tathmini ya hali yako ya sasa.  Jiulize maswali kuhusu maeneo gani unataka kuboresha au kubadilisha. Je, kuna mambo yanayokukwamisha au kukuzuia kufikia malengo yako? Kuelewa hali yako ya sasa ni hatua muhimu katika kuanza upya. 2. Weka malengo Weka malengo wazi na sahihi. Fikiria kwa kina kile unachotaka kufikia na kuamua hatua za kuifikia.  Malengo yako yanapaswa kuwa ya kusisimua, lakini pia yapaswa kuwa ya kufikika na yanayopimika.  Andika malengo yako na uwaeleze kwa uwazi. 3. Panga mpango wa utekelezaji Panga mpango wa vitendo wa jinsi utakavyotekeleza malengo yako. Tambua hatua ndogo na za kivitendo unazoweza kuchukua ili kufikia malengo yako.  Kwa kila hatua, weka muda uliopangwa na rasilimali zinazohitajika. 4. Jifunze kutokana na uz...

AGRICULTURE 101; KILIMO CHA TEMBELE

Habari   rafiki   mpendwa , Karibu   sana   katika   Makala   hii   Ya   Kilimo   na   Ufugaji Na   leo   tunakwenda   kuangalia   kuhusiana   na   Kilimo   Cha   Tembele. Mboga   nzuri   sana   na   inayopenda   na  kutumiwa   na    watu   wengi   sana   duniani Makala   hii   itakuwa   na   Sehemu/Vipengele   vifuatavyo; 1.Utangulizi 2.Aina za Tembele 3.Faida za Kiafya zitokanazo na Tembele 4.Namna Ya Kuandaaa Shamba 5.Kupanda 6 Kuvuna Karibu     sana    tujifunze   kuhusu    tembele. Kilimo cha tembele Kitaalamu    tembele   hujulikana   kama  ...

KARIBU KATIKA PROGRAM YA ELIMU KITAA(LEARNING SITE)

  Elimu Kitaa Foundation inakukakaribisha Katika Program ya Elimu Kitaa Habari ya kwako rafiki yangu. Bila shaka uko vizuri na unaendelea vyema na majukumu ya kila siku. Naitwa Joshua Golyama  mwanafunzi wa Shahada ya awali ya Sayansi ya Kilimo kwa Ujumla(Bsc.Agriculture General) kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine Cha Kilimo (SUA                                         Mwanzilishi wa Program inayoitwa ELIMU KITAA. Leo ninapenda kukuletea maeneo mbalimbali ambayo unaweza yatembelea na tukajifunza pamoja na mimi. Maeneo hayo utapata nafasi ya kusoma makala ambazo ninaziandika kila siku na kuziweka humo, na tukajifunza kwa pamoja na kupata maarifa zaidi na zaidi. Kwanza kabisa nikupe utangulizi wa maana halisi ya Neno hili ELIMU KITAA. Elimu Kitaa ni program inayohusika na kuandika makala mbalimbali katika mitandao ya Kijamii na kuandaa semina mbalimbali zenye kutupa maarifa muhimu san...