Maisha ya Mwanadam yamejaa maigizo , na wengi wao hawapendi kuishi maisha yao(uhalisia wao). Na kwa namna hii huwezi kufahamu mtu kwa undani vile alivyo.Kwa sababu anaweza kuigiza maisha yasiyo yake na ukamwamini. Lakini Wakati mzuri wa kumjua mtu vile alivyo ni pale anapopitia changamoto kubwa katika maisha yake. Hapo ndipo uhalisia wake huonekana, uimara wake, nguvu zake, akili zake na yote yanayomhusu Mwanafalsafa(Mstoa) aliwahi kusema maneno haya, " Difficulties are things that show a person what they are" __ Epictetus Akiwa na maana hii kwamba, magumu ni mambo ambayo yanamwonesha mtu jinsi alivyo. Zinapofika nyakati ngumu , ndipo ambapo tunaweza kumjua mtu vizuri na hiki ndicho kipondi kizuri sana ambacho kinamwonesha mtu vile alivyo. Kwa sababu wakati wa Raha mtu anaweza kuigiza na akafanikiwa kufanya hivyo. Ili kudhibitiisha uimara wako/kwamba umeimarika ni lazima magumu/changamoto uzipate ili kudhibitisha hi...
Hekima, Maarifa na Ufahamu Wekeza Saidia wengine