Nukuu kutoka kwa Steve Jobs.
" Our time is limited, so don't waste it living some one else's life.Do not be trapped by dogonas means living by using other people's thoughts , Don't let the noise of other people's opinion muffle your inner voice
The most important thing that have courage to follow your heart and mind some how they already know what you really must become .Every thing is of secondary importance".
Machache tunayojifunza kutoka katika Nukuu hii ni haya;
Muda wetu tulio nao ni mchache sana na yapo mengi sana ambayo yanatusubiri tuweze kuyafanya.Tunapaswa kuwa Makini sana tunapoendelea kwani Muda ni mchache.
Kwa kuwa muda muchache sana , tusiupoteze kwa kuishi maisha ya watu wengine. Tusiige maisha ya watu wengine, kila mmoja aishi maisha yake.
Fanya kile unachokiamini kwamba ni sahihi na kinakuletea Matokeo chanya katika maisha yako.
Usiishi kwa kufuata maoni/mapendekezo na mawazo ya watu wengine. Maneno ya watu yasikufanye ukaenda kinyume na kile unachokiamini katika Maisha Yako.
Jiamini wewe mwenyewe, Fuata kile akili yako na moyo wako vinakusukuma kufanya. Usifuate ushauri wa watu juu Ya Kile unachotaka kukifanya katika maisha yako.
ANGALIZO; Ushauri ni wa Muhimu sana, lakini sio kila Jambo unaweza kuomba ushauri.
Mfano; kama hujui nini cha kufanya kama vile kazi au biashara, usiombe ushauri kabisa .
Jua kwanza Biashara au Kazi gani unataka ndipo uombe ushauri .
Na mara upatapo ushauri huo, uchunguze kwa Makini ili kuona kama unaweza kukusaidia.UNATAKIWA KUWA MAKINI SANA HAPA.
Jambo La Muhimu zaidi ; Kujua hasa nini unataka au kuwa nani? Mengine yote yanafuatia baada ya hili la kwanza.
Jua kule unakokwenda, na vile unavyojiona hapo baadaye.
#Najifunza.
_____________________________________
Makala hii imeandikwa na ;
Joshua Golyama, ambaye ni Mwalimu, Mtaalamu wa Kilimo na Mifugo, Mhamasishaji Wa Mafanikio na Mwandishi.
+255 764 257 495 / +255 622 163 323
Barua pepe; golyamajoshua@gmail.com
Blogu; elimukitaa2020.blogspot.com
_____________________________________
Makala hii imeandikwa na ;
Joshua Golyama, ambaye ni Mwalimu, Mtaalamu wa Kilimo na Mifugo, Mhamasishaji Wa Mafanikio na Mwandishi.
+255 764 257 495 / +255 622 163 323
Barua pepe; golyamajoshua@gmail.com
Blogu; elimukitaa2020.blogspot.com
Comments
Post a Comment