Habari yako Rafiki Yangu Mpendwa;
Hakuna hata mmoja katika dunia anayeijua kesho yake, hata wasomi, wanasayansi na wataalam wote hapa duniani hili ni fumbo kubwa sana ambalo Mungu ametufumba sisi wanadam kesho yetu ni fumbo , na hakuna anayejua pia baada ya sekunde moja, dakika moja , siku moja au miaka kadhaa inayo kitatokea kitu gani? HAKUNA KABISA anayejua kesho au muda muchache ujao nini kitatokea.
Fumbo hili linatufundisha mambo mengi sana, na kutupa tahadhari kuhusu maisha yetu na mipango/malengo yetu tunayokuwa nayo.
Na fumbo hili linatupa mwongozo na hekima zaidi juu ya mambo tuyafanyayo .
Jifunze mambo yafuatayo na yatendee kazi , ukizingatia kwamba HAKUNA anayeijua kesho au muda muchache ujao nini kinaweza kutokea katika maisha yake
1. Usisubiri hadi uwe tayari ili kuanza kutimiza kusudi lako .
Anza hivyo hivyo ulivyo hata kama haujakamilisha mambo yote yanayohitajika .Hii itakusaidia na Kuishinda roho ya kukata tamaa.
KUMBUKA; muda huu haukusubiri wewe ili uwe tayari, kadiri upatavyo nafasi , tumia vyema nafasi hiyo uliyoipata na nguvu zako zote
2.Hakikisha unatumia Muda vizuri ili usije kujuta hapo baadaye na kuanza kusema kuwa Muda ni Mchache. " Mambo mengi muda muchache"
Shughulika na wekeza nguvu zako zote kwa mambo machache yaliyo na umuhimu kwako ili kuzuia kupoteza muda kwa mambo mengi yasiyo na umuhimu kwako.
3 .Fanya kazi kwa bidii na kwa ubora wa hali ya juu sana kwa kila ukifanyacho.
Fanya kazi kama ndiyo siku yako ya mwisho kuishi duniani _ Hii itakusaidia na kukuhamasisha Kusonga mbele zaidi .
4.Ishi leo kwa kuwa hujui kesho yako itakavyokuwa Leo yako unaifahamu na kesho yako huijui,hivyo itumie leo yako vyema.Usiseme nitaanza kesho HAPANA, anza leo na usisubiri Kesho Kwa maana huna uhakika nayo.Muda sahihi na muafaka wa Kutimiza malengo yako ni SASA na siyo baadaye au kesho.
5.Maisha hayakusubiri wewe ili uwe tayari , Maisha Yataendelea kwenda, dunia itaendelea kwenda kwa sababu haijali kama upo tayari au umeshakuwa tayari.
Anza kidogo na kile ulichonacho, kuanza ni bora kuliko kuanza kabisa.Usiseme kwamba ngoja nisubiri hadi nitakapokuwa na Umri fulani.Muda na maisha havikusubiri wewe kuwa tayari
Anza kidogo kidogo huku ukishafanya kwa Umakini, na uaminifu mkubwa.
Hakuna mtu yeyote aliyefanikiwa, aliyeibuka na kuwa na mafanikio hayo aliyonayo, bila shaka alianza mbali sana kuwa kuanza kidogo kidogo na kufanya kazi kwa bidii, hatimaye kufika hapo walipofikia.
6.Kama kuna kitu/jambo ambacho unatakiwa kuwa na UBAHILI nacho, basi ni muda wetu.
Watu wengi tumekuwa tunaruhusu mtu yeyote kutumia muda wetu, na kuanza kuwalalamikia wengine kwamba wanatupotezea Muda.Hupaswi kumlaumu mtu yeyote yule, kabla kuwalaumu wengine jlaumu wewe mwenyewe kwanza kwa kutokuwa makini na muda ulionao.
Wengi wetu tunautumia muda vibaya (hovyo)hasa kwenye starehe.
Kuwa BAHILI wa muda usiruhusu mtu yeyote kuutumia muda wako kwa namna yeyote ile.Tumia muda wako katika mambo ya muhimu na Msingi sana katika maisha yako.
7. Ishi leo kama ndiyo siku yako ya mwisho;
Chukulia kila siku kama ya mwisho , fanya yale ya muhimu pekee Maana *IPO SIKU HAITAKUWA NA KESHO. Hivyo usiseme nitafanya KESHO fanya SASA.
8. Kuahirisha mambo ni moja ya upotevu wa muda,
Watu wengi huwa tunaahirisha mambo yale ambayo tumeyapanga bila kujua madhara yake. Unapoahirisha kufanya unakuwa unapoteza muda kwa sababu unapoahirisha kitu(jambo) siyo tu unapoteza muda wa SASA, bali unapoteza na muda ujao ambao huna uhakika nao.
Hivyo, ni vyema sana ukajitahidi kulifanya jambo ambalo umelikusudia kulifanya na usipende kuahirisha kila jambo unalolipanga.Hakikisha huruhusu sababu yoyote kukufanya uahirishe jambo ulilolikusudia.
Chagua sasa yale mambo yaliyo ya muhimu na umuhimu mkubwa kwako na tumia nguvu , juhudi na muda wote kushughulika nayo.
Mwisho; tunaposoma Maandiko Matakatifu tunapata jambo kubwa sana ambalo linakamilisha makala hii ya leo
Mhubiri 9:10 "Lo lote mkono wako utakalolipata kulifanya, ulifanye kwa nguvu zako; kwa kuwa hakuna kazi, wala shauri, wala maarifa, wala hekima, huko kuzimu uendako wewe."
Kila jambo unalolifanya lifanye kwa nguvu zako zote, na utafanikiwa.
Mungu akubariki sana.
Ahsante.
Makala hii Imeandikwa na;
Joshua Golyama
Mwanafunzi Wa shahada Ya awali ya Sayansi Ya Kilimo
Chuo Kikuu Cha Sokoine cha Kilimo (SUA-MOROGORO)
+255764257495
Barua pepe; golyamajoshua@gmail.com.
Blogs; elimukitaa2020.blogspot.comHakuna anayeijua Kesho;Hili ni fumbo tulilofumbiwa wanadam
Comments
Post a Comment