Maisha ya Mwanadam yamejaa maigizo , na wengi wao hawapendi kuishi maisha yao(uhalisia wao). Na kwa namna hii huwezi kufahamu mtu kwa undani vile alivyo.Kwa sababu anaweza kuigiza maisha yasiyo yake na ukamwamini.
Lakini Wakati mzuri wa kumjua mtu vile alivyo ni pale anapopitia changamoto kubwa katika maisha yake. Hapo ndipo uhalisia wake huonekana, uimara wake, nguvu zake, akili zake na yote yanayomhusu
Mwanafalsafa(Mstoa) aliwahi kusema maneno haya,
" Difficulties are things that show a person what they are" __ Epictetus
Akiwa na maana hii kwamba, magumu ni mambo ambayo yanamwonesha mtu jinsi alivyo.
Zinapofika nyakati ngumu , ndipo ambapo tunaweza kumjua mtu vizuri na hiki ndicho kipondi kizuri sana ambacho kinamwonesha mtu vile alivyo. Kwa sababu wakati wa Raha mtu anaweza kuigiza na akafanikiwa kufanya hivyo.
Ili kudhibitiisha uimara wako/kwamba umeimarika ni lazima magumu/changamoto uzipate ili kudhibitisha hilo.
Utawafahamu marafiki wa kweli pale ukikutana na magumu.
Utajua na kugundua uwezo wako na kukabiliana na changamoto, pale utakapozipata
Utajua uwezo wako wa kuzuia hisia ya Hasira pale ndugu, rafiki na mtu yeyote anapokuudhi
Hata kiongozi bora uwezo wake hujulikana pale magumu anapoyapata, na sio wakati wa Amani .
Hatua ya Kuchukua; Unapopitia magumu, jitie nguvu na jiambie kuwa hayo ndiyo yanayokuonyesha vile ulivyo.
Hivyo pambana na hakikisha unashinda vyema katika changamoto unayokutana nayo.
#Najifunza.
_____________________________________
Makala hii imeandikwa na ;
Joshua Golyama, ambaye ni Mwalimu, Mtaalamu wa Kilimo na Mifugo, Mhamasishaji Wa Mafanikio na Mwandishi.
+255 764 257 495 / +255 622 163 323
Barua pepe; golyamajoshua@gmail.com
Blogu; elimukitaa2020.blogspot.com
Comments
Post a Comment