Habari rafiki mpendwa;
Ni matumaini yangu u mzima na unaendelea vyema na majukumu yako ya kila siku , hongera kwa yote na endelea zaidi ili tuweze kufikia mafanikio makubwa zaidi
Karibu sana katika mtandao huu wa ELIMU KITAA(STREET EDUCATION) ambao unahusika na kutoa elimu kwa njia ya makala kuhusu mambo mbalimbali kama vile , Kilimo, Afya, ufugaji, Mafanikio binafsi , na makala zinazoelimisha zaidi kuhusu kulijua Kusudi la Mungu katika maisha yako, pia Mtandao huu unahusika pia kutoa makala zinazohusu Elimu ya Lishe na Matumizi ya Muda.
Lengo kuu la mtandao huu ni kushirikisha na kutoa maarifa sahihi kwa watu wote kuhusu maduala yote tunayokutana nayo katika maisha.
Huo ni utangulizi kiufupi kuhusu mtandao huu ,
Sasa nikukaribishe katika makala Ya AGRICULTURE 101 , ukurasa unaohusu masuala yot yanayohusu kilimo na mifugo,
Leo tunakwenda kujifunza kiufupi kuhusu ufugaji bora kwa Kuku wa Mayai .
Katika ufugaji wa aina mbili ambao unajulikana na kila mtu , ufugaji wa kuku wa mayai na ufugaji wa kuku wa nyama.
Tunakwenda kujifunza kiufupi, kuhusu kanuni za msingi za kuzingatia katika ufugaji wa Kuku wa Mayai na makal zijazo zitakuwa na maelezo ya kutosha zaidi kuhusu ufugaji wa kuku wa Mayai .
Kwanza kabisa , unachotakiwa kufahamu ni kuwa;Ili uweze kuwa na ufugaji bora na wenye tija zipo Kanuni chache za Kuzingatia, ambazo ni;
1.Kuchagua aina nzuri ya mnyama/ndege unayetaka kumfuga-Hii inategemea na mahitaji yako/malengo ya ufugaji , na mazingira uliyopo
2.Lishe bora.
3.Kutibu na kudhibiti Magonjwa
4 .Mazingira safi /mahali pa kuishi
Baada ya kujua Kanuni za Msingi katika ufugaji , Karibu tuendelee na Mafunzo yetu
Faida zinazopatikana kutokana na ufugaji wa kuku wa mayai
1. Huwapatia wafugaji lishe bora kwa kula baadhi ya mayai .
2.Huinua kipato cha kaya na familia kwa kuuza mayai ambayo hutagwa kwa wingi na kwa kila siku.
3. Hutoa ajira kwa watu wengi ambao huendesha shughuli zao kwa kufuga kuku wa mayai .
4. Humpatia mfugaji /mkulima mbolea ya kulimia na kukuzia mazao bustanini au shambani (kinuesi cha kuku).
5. Humpatia mfugaji fedha kutokana na mauzo ya mbolea , mauzo ya kuku ambao wameshakomaa kwa kutaga .
6. Humpatia mfugaji kitoweo kutokana na kuwachinja kuku waliokomaa kutaga .
7. Humpatia mkulima fedha kutokana na mauzo ya manyoya ya kuku waliochinjwa kwa ajili ya kutengeneza mito na mapambo .
KANUNI ZA UFUGAJI BORA WA KUKU WA KISASA WA MAYAI .
1.Kwapa kuku malazi bora kwenye banda zuri
(a) Vifaranga
_Andaa na safisha chumba cha kuwalelea , paa na kyta na sakafu
_ Tandaza pumba za mpunga au takataka za randa ambazo ni kavu na safi sakafuni
_Andaa mviringo wa kulelea vifaranga ili uwazuie wasizurure mbali na chanzo cha joto
_Ning'iniza balbu ya umeme au taa ya chemli ndani ya mviringo ili kuwapa vifaranga joto .
_Hakikisha banda lina hewa ya kutosha lakini haliingizi upepo mkali . Upepo na jua kali vinaweza kuvidhibiti kwa kuweka mapazia dirishani
(b) Kuku wakubwa .
_ Waandalie banda lenye sifa za vifaranga lakini usiwawekee mviringo wala chanzo cha joto.
_Wawekee vitundu au maboksi ya kutagia na majukwaaa ya kusimamia ya miti au mbao.
_Wawekee vitundu au maboksi ya kutagia na majukwaaa ya kusimamia ya miti au mbao.
2. Kuchagua kampuni yenye vifaranga bora wa mayai
Zipo kampuni nyingi ambazo ni maarufu kwa uuzaji wa vifaranga .Hata hivyo waone wafugaji maarufu na wafugaji wenye wazoefu wa kufuga kuku wa mayai pamoja na wataalamu wa mifugo wa kuelekeze kwenye kampuni ambazo vinauza vifaranga bora.
3. Matunzo bora kwa kuwapa chakula bora , dawa , na maji wakati wote.
(a) Matunzo kwa vifaranga
_Andaa chakula cha vifaranga
_Andaa maji safi na salama
_Safisha vyombo vya kulishia na kunywesha
_Andaa dawa ya kudhibiti magonjwa na vimelea
_Weka mviringo ndani ya banda , vyombo vya kulishia na kunyweshea ndani ya mviringo .
_Washa taa au balbu iliyoning'inizwa katikati ya mviringo.
_Weka maji kwenye chombo cha maji na chakula kwenye chombo cha chakula
_Watoe vifaranga kwenye maboksi uwainginize ndani ya mviringo
_Wapatie chakula cha kutosha mara mbili kwa siku
_Wapatie maji safi na salama ya kutosha mara mbili kwa siku .
_Hakikisha hoto halipungui kwenye 32c na halizidi 35c Pandisha balbu juu kupunguza joto au shusha balbu ili kuongeza joto.
_Panua mviringo Kulingana na kasi ya kukua kwa vifaranga wako, Wanapitimiza mwezi mmoja .
_Usisahau kuweka kumbukumbu ya :-
Tarehe na idadi ya vufaranga vilivyonunuliwa
Idadi ya vifo, tarehe na sababu ya vifo vyao
Idadi ya waliopo
Kama ulitokea ugonjwa , andika dawa iliyowaponya
Kiasi cha chakula unachowalisha kila siku
(b) Matunzo kwa kuku wanaokua.
_Jinsi kuku wanvyoendelea kukua ndivyo wabavyopunguza ulaji wa chakula .Wape kuku wa mwezi mmoja hadi minne chakula cha kukuza kama kama kilo 28 kwa siku kwa kuku 100.Wape maji safi na salama ya kutosha
_Wape kuku wanaotaga chakula cha kutosha yaani kilo 15 hadi 18 kwa siku kwa kuku 100..Wapatie maji safi na salama ya kutosha na ikiwezekana wapatie vitamini na madini maalumj kwa ajili ya kuku.
4. Usafi wa vyombo vya chakula na maji
Vyombo hivi vinatakiwa vitunzwe katika hali ya usafi .Kinyume cha hivyo huweza kuwa ni chanzo kikuu cha Magonjwa mbalimbali.
(i)Hakikisha chombo cha kunyweshea maji hakivuji ili kisije kikalowanisha pumba na sakafu.
(ii)Hakikisha chombo cha chakula nacho hakijatoboka popote ili kisije mwaga chakula hasa kwa vile vinavyotundikwa .
(iii) Wakati wa kuwawekea kuku chakula , na maji , mwaga mabaki kisha safisha na kukausha vyombo ndipo uweke chakula na maji.
(iv) Ni vyema uwe na vyombo zaidi ya seti moja ili viweze kutumika wakati vingine vikikauka juani.
5. Usafi wa banda na mazingira ya ndani ya banda. Tahadhali za hali ya juu zisipo chukuliwa kulinda usafi katika banda, kuku wanaweza wakapata matatizo ya kyshikwa na Magonjwa mbalimbali.Hivyo basi;
(1) Hakikisha banda halina vumbi na tando za buibui kwa wingi
(2) Hakikisha Pumba au takataka za randa ulizotandaza sakafuni hazilowi na maji na kama zikimwagikiwa na maji kwa bahati mbaya, ziondolewe na kuwekwa pumba nyingine kavu na safi
(3) Pumba zikishakaa kwa muda mrefu bandani hulowanishwa na vinyesi vya kuku, na huchafua miguu ya kuku .Hivyo basi hakikisha unabadilisha pumba kabla hazijalowana sana .
Makala hii itaendelea....
Makala hii imeandikwa na;
Joshua Golyama
Mwanafunzi wa Shahada Ya Awali ya Sayansi Ya Kilimo
Chuo Kikuu cha Sokoin Cha Kilimo (SUA-MOROGORO)
+255764257495/0622163323
Baruapepe;golyamajoshua@gmail.com
Blogu; elimukitaa2020.blogspot.com
Comments
Post a Comment