Skip to main content

Posts

JENGA TABIA YA KUJIFUNZA KILA WAKATI , ONDOA KIBURI KATIKA KUJIFUNZA.

JENGA TABIA YA KUJIFUNZA KILA WAKATI ,  ONDOA KIBURI KATIKA KUJIFUNZA. Unapokosa tabia ya kujifunza na kuwa na hali ya kujiona unajua kila kitu utakuwa nayo na Kwa Maana Hiyo hautaweza kuwa na spirit ya kuendelea kujifunza zaidi na zaidi. Lakini unapokuwa unajifunza kila wakati, utagundua kwamba Mambo mengi huyajui hii itaamusha Nguvu mpya, ari mpya na hamasa ya kue ndelea kujifunza zaidi. Jifunze zaidi ili upate hamasa ya kujifunza zaidi. Na MUHIMU,  ili uweze kujifunza ni lazima ujione hujui , na kama utaona kama unajua kamwe hautaweza kujifunza Kwa maneno Mengine unakuwa na KIBURI KATIKA KUJIFUNZA ambacho Kinakuzuia wewe kujifunza zaidi, kwa sababu ndani yako kutakuwa na Sauti kama hii  'mbona kila kitu ninakijua, kujifunza ni kupoteza muda' Hakikisha unajitahidi unakuwa na Tabia Ya KUJIFUNZA, kwa sababu katika Karne hii Ya 21 kuna Maendeleo makubwa sana Ya Teknolojia na Ni ULIMWENGU WA TAARIFA hivyo usipojifunza kamwe hauwezi kuwa na Taarifa sa...

HEKIMA YA SIKU; Kila Jambo ulifanyalo lifanye kama wajibu na si kutegemea shukrani au kutambulika

Kila jambo unalolifanya, lifanye kama wajibu, na usifanye ukitegemea kutambuliwa, au kupewa shukrani. Watu wengi  wanapata shida sana  pale ambapo wanafanya mambo mengi, na hakuna anayeonekana kuwashukuru kwa yale wanayoyafanya. Unajitoa kwa nguvu zako kuhakikisha kila kitu kinakuwa sawa. Fuatilia mifano hii michache ili uweze kupata kile ninachokimaanisha hapa; Mfano  wa kwanza; Viongozi mbalimbali tulio nao, wanatumia muda wao mwingi na nguvu nyingi kuhakikisha wale wanaowaongoza wanafika pale wanapotakiwa kuwa. Na  hakuna hata mmoja anayetambua mchango wao na nguvu zao walizotumia kuwaongoza. Na pengine asiwepo hata mmoja wa kusema asante kwa yale wanayafanya. Mfano wa Pili ; kwenye mahusiano,unakuta boyfriend/girlfriend anafanya kila anachoweza ili kuboresha mahusiano yao, kumsaidia kwa kila hali/changamoto anayoipitia Lakini haoni mwenzie akimshukuru au kutambua kwa kile anakifanya. Mfano wa tatu; Kazini kwako, unafanya kila kitu vile inavyotaki...

KUWA MAKINI SANA NA NAMNA UNAVYOTUMIA MUDA WAKO

KUWA MAKINI SANA NA NAMNA UNAVYOTUMIA MUDA WAKO "Muda ni wa thamani sana kuliko fedha , unaweza kuzipata fedha kila siku Lakini muda hauwezi kuupata ukishaupoteza. Hivyo, tunatakiwa muda vizuri ule tunaoupata na kwa umakini mkubwa zaidi. Epuka kupoteza muda kwa kutofanya yale yasiyo na umuhimu kwako. Maana wengi tunahangaika na mambo mengi sana ambayo hayana mchangi wowote katika maisha yetu. Pale upatapo nafasi ya kufanya jambo, hakikisha unalikamilisha na kwa usahihi kabla ya kuanza kufanya jambo jingine. Wekeza muda wako kwa kujifunza zaidi , wekeza zaidi ndani yako, ilishe akili yako maarifa mapya kila siku ili kuweza kuwa na mabadiliko makubwa hapo baadaye. Wekeza ndani yako kwa kusoma vitabu, kusoma Makala na kuhudhuria semina mbalimbali Jifunze kila siku na hii ni ni namna sahihi ya kutumia muda wako Vizuri. Huwa napenda kusema kuwa, watu wengi tunalalamika na kukiri kwamba " muda mchache , na Mambo mengi, Swali langu ni hili Je,  hayo Mengi uliyo nayo...

KITABU CHA JUMA; My Philosphy For Successful Living -Falsafa Yangu Ya Maisha Ya Mafanikio.

KITABU CHA JUMA; My Philosphy For Successful Living -Falsafa Yangu Ya Maisha Ya Mafanikio. Habari ya kwako rafiki mpendwa, Natumai umekuwa na wiki ya baraka sana na bila shaka umepiga hatua kadhaa zenye kukusaidia katika safari hii tuliyonayo ya kulikamilisha kusudi la Mungu katika maisha yetu. Nikukaribishe katika makala hii ya kitabu cha Juma,  kutoka katika Kitabu Cha My Philosophy For Successful Living-Falasafa yangu ya Maisha Ya Mafanikio kilichoandikwa na Jim Rohn Jim Rohn ni Mjasiriamali wa Marekani, Mwandishi, na mhamasishaji Katika Juma hili tunakwenda kujifunza mambo machache na ya muhimu sana kutoka katika Kitabu hiki  cha My Philosophy For successful living Karibu sana tujifunze kwa pamoja mambo haya ambayo mwandishi anatufundisha katika kitabu hiki Kila mmoja wetu anatamani kuwa na maisha mazuri, hakuna hata mmoja anayetamani kuishi maisha ya shida. Lakini kutokana na ujinga wetu wa kutofahamu kanuni za Msingi za kuwa na maisha mazuri tunaishia k...

KUTOA KAFARA ILI UWEZE KUWA NA MAFANIKIO MAKUBWA.

Bila shaka kichwa cha mada hii kinakuchanganya na unashindwa kuelewa nini nimedhamiria  kukuambia, Lakini ambatana nami hadi mwisho mwa Makala hii utaelewa maeneo halisi ya mada hii ya leo. Karibu sana tujifunze pamoja ili tupate Maarifa ya kutusaidia. Wakati naendelea kusoma vitabu mbalimbali, nilikutana na jambo hili ambalo lilinishangaza kidogo, lakini nilijifunza mambo mengi sana muhimu katika safari ya mafanikio. Nimeyasoma na kujifunza kutoka kitabu cha K WANINI HADI WEWE SIO TAJIRI   kilichoandikwa na Kocha Makirita Amani Nimeamua nikushirikishe maarifa haya nawe upate kujifunza , na kuchukua hatua ya kuyafanyia kazi. Mwandishi anaanza kwa kueleza yafuatayo;  Huwezi kufikia utajiri mkubwa na mafanikio kwenye maisha bila ya KUTOA KAFARA. Mwandishi anaeleza dhana ya TRADE OFF akiwa na maana kwamba " Kupoteza kitu fulani ili kupata kitu kingine , au kuliwa eneo fulani ili uweze kula eneo jingine  Kafara anayozungumzia mwandishi...

KITABU CHA JUMA; My philosophy for successful living-Falsafa Yangu ya Maisha Ya Mafanikio Kilichoandikwa na Jim Rohn

KITABU CHA JUMA;  My philosophy for successful living- Falsafa Yangu ya Maisha Ya Mafanikio  Kilichoandikwa na Jim Rohn. Moja ya jambo muhimu sana katika dunia hii ya sasa ni kujifunza, ili kuweza kuwa bora zaidi katika jambo lolote huna budi kuwa na tabia ya kujifunza,  Kupitia kujifunza tunapata maarifa ambayo yanaweza kutuvusha hatua moja kwenda hatua nyingine. Kufikia mafanikio makubwa sana katika maisha hatuna budi kujifunza kila siku Watu wengi ambao wamefanikiwa wana tabia moja muhimu sana ambayo ni Kujifunza kila wakati na kila siku, shauku yao kubwa ni kujfunza na kujua mambo mengi ambayo yanawasaidia kukua zaidi  Kupitia kujifunza, unapata nafasi ya kuyajua mambo mengi sana katika maisha.Hatuwezi kuyajua yote lakini tunatakiwa kujua mambo mengi. Kama utapata nafasi ya kuwafutilia sana wale wanaojua mambo mengi katika Jamii , wana tabia ya kujifunza kila siku na kila wakati. Hivyo, kama tunataka kufikia mafanikio makubw...

KARIBU KATIKA MTANDAO WA ELIMU KITAA (STREET EDUCATION); Tujifunze kwa pamoja, ili tupate maarifa sahihi ya kutusaidia katika maisha yetu.

                                                  Rafiki yangu mpendwa; Ni matumaini yangu kuwa unaendelea vizuri na majukumu ya kila siku na unaendelea kufanya kazi kwa bidi ili kuwa na maisha bora sana. Moja ya kitu cha msingi sana katika maisha ambacho hutakiwi kukiacha ni kujifunza kila siku na kutafuta kuwa bora zaidi. Maisha ni sanaa, na kama ilivyo sanaa inahitaji ubunifu kila siku, usipotaka kujifunza kamwe hauwezi kuwa mbunifu. Hivyo, katika maisha hutakiwi kuacha kujifunza ili uweze kuwa bora zaidi. Karibu sana katika Makala hii ambayo ni muhimu sana kwako na nimeifanya kuwa maalumu sana, kwa sababu nimekuandalia na kukuletea Makala hii ili uweze kujua hasa kwa undani kuhusu Mtandao huu wa Elimu KItaa (Street Education) chanzo chake, unahusika na nini, malengo yake na nini utakipata katika mtandao huu. Karibu s...