George Bernard Shaw aliwahi kusema maneno haya......"beware of false knowledge, it is more dangerous than ignorance" Kwamba "Kuwa makini sana na taarifa zisizo sahihi, kwa sababu ni hatari zaidi kuliko ujinga" Taarifa ni kitu cha msingi sana, unapohitaji kufanya jambo fulani. Ukweli ni kuwa unahitajika kuwa na taarifa nyingi, kabla ya kufanya jambo. Lakini taarifa hizo lazima ziwe sahihi sana, kwa sababu zisipokuwa sahihi zitakupelekea mahali pabaya. Ili ufanye vyema katika jambo fulani, unalazimika kuwa na taarifa nyingi na zilizo sahihi. Kuwa makini sana na vyanzo vya taarifa yako Fanyia tathmini kwanza, juu ya chanzo cha taarifa, Je, ni sahihi na zitakufaa. Kumbuka, Maamuzi yoyote yale yanategemea taarifa ulizo nazo. Kufeli au kufanikiwa kunategemea na taarifa ulizo nazo. Kiwango cha usahihi wa taarifa huamua aina ya matokeo ambao unakwenda kuyapata. ..Wito wangu ni kuwa, tuko katika karne ya TAARIFA, karne ambayo walio na taarifa sahihi ndio wanaofanikiwa. Na...
Hekima, Maarifa na Ufahamu Wekeza Saidia wengine