Nyuma Yako liko kundi kubwa sana la watu wanaojifunza kutoka kwako, Yaani wanafuata vile wewe unavyofanya .
Ukifanya , nao wanafanya na Usipofanya nao hawafanyi pia
Ki-ufupi wewe Ni Kiongozi wa Kundi kubwa sana La Watu USILOLIJUA .
Hivyo pale unapoacha kufanya Kile ulichoanza kufanya, Unapo KATA TAMAA , na wao pia wanashindwa kuendelea kwa sababu kiongozi wao umekata Tamaa.
Usikate Tamaa, Usivujike Moyo na Kurudi Nyuma , Kwani lipo Kundi kubwa La watu usilolijua wanaanguka baada Ya wewe KUKATA TAMAA.
Usikate Tamaa , Songa Mbele na Fanya Kiume Uwe Hodari Kwa FAIDA YAKO na WALE WOTE WANAOJIFUNZA KUTOKA KWAKO( KUNDI KUBWA LA WATU USILOLIJUA ) .
Kabla Hujakata TAMAA, Kurudi Nyuma na Kuacha Kabisa KUMBUKA hili , itakusaidia Kuendelea Mbele zaidi.
Kwa kuwa lipo kundi kubwa linakufuatilia, fanya vile bora na kwa umakini wa hali ya juu sana.
Usikate tamaa, Songa mbele kwa ajili ya Faida ya Wengine, hata kama unataka kukata usifanye hivyo kwa sababu unakwenda kuangusha kundi kubwa la watu
#Najifunza.
_____________________________________
Makala hii imeandikwa na ;
Joshua Golyama, ambaye ni Mwalimu, Mtaalamu wa Kilimo na Mifugo, Mhamasishaji Wa Mafanikio na Mwandishi.
+255 764 257 495 / +255 622 163 323
Barua pepe; golyamajoshua@gmail.com
Blogu; elimukitaa2020.blogspot.com
Comments
Post a Comment