Zipo kanuni nyingi sana ambazo Waandishi wameandika na kufundisha kuhusu kufanikiwa katika kila jambo tunalolifanya, Kila mmoja ameandika kwa namna ile ambayo ziliweza kumsaidia.
Lakini ipo Kanuni moja na Ya Msingi sana katika safari ya Mafanikio nayo ni NIDHAMU BINAFSI.
Kanuni hii ni kama kanuni kiongozi ambayo bila ya kuwa nayo hatuwezi kufanikiwa .
Nidhamu ni tabia ngumu kuijenga katika maisha ya Mwanadamu na Pia ni tabia ambayo ukiwa nayo unaweza ukafanikiwa kwa Haraka sana.
'Nidhamu ni uwezo wa mtu kufanya jambo fulani analopaswa kulifanya kwa wakati sahihi ikiwa anapenda au hapendi.
Nidhamu ni nguvu inayotusukuma kuendelea zaidi.
Karibu tujifunze kwa pamoja kuhusu namna gani tunaweza kujijengea nidhamu ya kufikiri kwa usahihi zaidi katika maisha ya Kila siku.
Moja ya nidhamu ngumu kuijenga katika maisha ni nidhamu ya kufikiri.
Hapa tunawapata watu wa aina tatu kuhusu kufikiri; wapo wale wanaofikiri, wapo wanaofikiri kuwa wanafikiri, na wapo ambao wako tayari kufa kuliko kufikiri.
Hivyo kufikiri ni tabia ngumu ambayo watu wengi hatupendi kuifanya na wakati mwingi inatugharimu sana katika kuchukua maamuzi , tunachukua maamuzi kulingana na hisia na si katika uhalisia wenyewe.
Fanya yafuatayo ili kujijengea nidhamu ya kufikiri kwa usahihi;
- Pata muda wa kufikiri na kutafakari kuhusu mambo muhimu na matatizo mbalimbali unayokutana nayo katika maisha. (hali uliyo nayo sasa
- Hakikisha unapata utulivu wa kutosha kwa dakika 30-60 utumie kwa ajili ya kufikiri na kutafakari kuhusu mambo mbalimbali. Uwe na desturi ya kukaa peke yako kwa muda fulani, mahali ambako kuna utulivu wa kutosha.
- Kukaa peke yako na kwa utulivu mkubwa , huamsha ufahamu wako na kuweza kuyaelewa mambo mbalimbali kwa urahisi zaidi na kufikia maamuzi mazuri.
- Kulifanikisha hili, hakikisha unakuwa na diary, notibuku au kidaftari kidogo ambacho unakitumia kutunzia Kumbukumbu, andika kila jambo unalolipitia katika maisha yako/hali uliyo nayo kwa sasa. Na kufanya hivi kunakusaidia sana kupata mawazo mapya yaliyo ya msingi sana .
- Aristotle alisema kuhusu Hekima ( uwezo wa kuwa maamuzi mazuri) ni mjumuisho wa uzoefu na kutafakari(reflection). Kadiri unavyotafakari na kufikiri zaidi kuhusu uzoefu wako, ndipo unapojifunza zaidi na kuyafahamu mambo mengi zaidi.
- Fanya mazoezi kwa dakika 30-60 kila siku, Wakati unapoendelea kufanya mazoezi unapopata mawazo mapya na kufanya maamuzi mazuri.
Hekima = Uzoefu + Kufikiri
Ili kuweza kuchukua maamuzi yaliyo bora zaidi(sahihi) katika maisha yako ni lazima uwe na tabia ya Kufikiri Kwa umakini.
Watu wengi tunaendeshwa na hisia na si kwa kufikiri na kufikia maamuzi sahihi
Hatua ya Kuchukua;
Jenga nidhamu hii ya kukaa peke yako na kufikiri kwa umakini sana kuhusu maisha yako na jambo lolote unalotamani kulifikia katika maisha. Unapokuwa peke yako unapata mawazo mapya na kufikia hitimisho lilio sahihi juu ya jambo lolote.
Fikiri kabla ya kutenda, Usiendeshwe na hisia bali chukua maamuzi yaliyo bora zaidi.
Maamuzi ya haraka huwa ni maamuzi yasiyo sahihi,
#Najifunza.
_____________________________________
Makala hii imeandikwa na ;
Joshua Golyama, ambaye ni Mwalimu, Mtaalamu wa Kilimo na Mifugo, Mhamasishaji Wa Mafanikio na Mwandishi.
+255 764 257 495 / +255 622 163 323
Barua pepe; golyamajoshua@gmail.com
Blogu; elimukitaa2020.blogspot.com
Comments
Post a Comment