Skip to main content

Ifahamu siri hii ili uweze kufanikiwa zaidi katika maisha yako


Je, umewahi kujiuliza kwanini watu wengi wanaanza biashara na baada ya muda mfupi wanaacha?
Na Kwanini biashara za watu fulani zinakuwa na wateja wengi kuliko biashara zingine 
Nini siri ya Haya yote?

Karibu tujifunze kwa pamoja ili tupate  majibu ya maswali yetu tunayojiuliza .
Jibu la swali letu kwa nini biashara nyingi zinakosa wateja na zingine kuwa na wateja wengi ni UBORA na THAMANI inayotolewa na Biashara husika.

Katika biashara yoyote ile yako mambo mawili makubwa ambayo wateja wanayaangalia.
1.Unafuu wa bei
2.Ubora wake.
Wateja wanataka kitu  chenye bei rahisi na pia ambacho kina ubora.

Ukweli ni kwamba katika nyakati hizi za utandawazi  hakuna baishara mpya  au chochote kipya ambacho unaweza kukifanya.
Karibia kila kitu wapo watu wanakifanya.
Na hauwezi ukasema kwamba unaenda kufanya jambo jipya kabisa ambalo halijwahi kufanyika  

Kila kitu/biashara wapo watu wanaoifanya baishara hiyo.Hivyo hauko peke yako unayeendesha biashara hiyo.
Ubora wako na thamani unayoitoa kwa wateja wako ndiyo itakayokufanya biashara yako kuendelea zaidi.

Mfano; wafanya baishara wawili wanaofanya baishara zinazofanana(bidhaa sawa), kitakachokwenda kuwatofautisha hapo in ule ubora wa bidhaa na thamani ambayo  kila mmoja anayo litoa kwa wateja wa biashara hiyo.

Hata kama unafanya biashara inayofanana na mtu mwingine, tafuta kuwa tofauti naye kwa kuongeza thamani na ubora zaidi katika biashara yako.

Wanachokihitaji wateja ni Ubora na Thamani Kubwa ambayo unaitoa kwa wateja wako
Kama bidhaa zako  hazina  ubora, hakuna atakayekuja kununua.

Hii inajumuisha pia maisha ya kila siku na vile viti ambavyo tunavifanya kila siku 
Lazima tuvifanye katika ubora wa hali ya juu sana.
Kinachotafutwa sasa ni ubora ulio nao .

Mhitimu anayetakiwa na anayetafutwa kuajiriwa si yule aliyefaulu pekee, bali mwenye elimu yenye ubora .
Kama elimu yake haina ubora hawezi kupata kazi.
Kila jambo linalofanyika linatakiwa kufanyika katika ubora.

Wanaohitimu vyuo vikuu na vyuo hapa nchini wako wengi sana, na kuna idadi kubwa sana ya wahitimu ambao wamesoma kitu kimoja na wote wanataka wakapate kazi.

Haitawekana kwa wote kupata kazi, ila kinachokwenda kuwatofautisha ni Ubora wa Elimu yao 
Kampuni na taasisi mbalimbali zinahitaji kufanya na mtu aliye bora zaidi.


Najua hata wewe unapoenda sokoni/dukani kununua baadhi ya mahitaji ya nyumbani, unatafuta kilicho bora.
Kumbe , kwa ulimwengu wa sasa kinachotafutwa sana ni Ubora na Uthamani ulio nao.

Hata kama utakuwa na baishara nzuri na kubwa kiasi gani, kama haina ubora hiyo haifai na haiwezi kudumu kwa muda mrefu .

Hata viongozi wanaochaguliwa , wanatakiwa kuwa bora na ndivyo ambavyo watu wanataka watu wa aina hiyo.
Bila ya kuwa bora hauwezi kuwa kiongozi, bila ya kuwa bora baishara yako haiwezi kuendelea mbele zaidi.

Kwa maelezo hayo mafupi, nadhani umejifunza kitu kuhusiana na Ubora na umuhimu wake katika biashara na maisha ya kila siku.

Kwa kila jambo unalolipata kulifanya, lifanye katiak ubora.
Usifanye ili kumaliza, hapana bali fanya katika ubora .Ni heri ukatumia muda mwingi kulifanya jambo kwa ubora zaidi kuliko ukaliharakisha jambo na likose ubora .

Hata kama unafanya kazi ya mtu, labda umeajiriwa kufanya kazi katika kampuni fulani, mtumishi wa umma/serikalini  na katika eneo lolote like hakikisha unalifanya katika ubora unaotakiwa.

Ukiwa bora katika jambo lolote unalolifanya , hakuna atakayekuzuia kutolipwa zaidi na kukua zaidi.

"If you become good at what you do, there is nothing that can stop you from getting paid more and promoted very faster"__Dan Kenedy

Ukiwa vizuri katika eneo lolote lile, hakuna atakayekuzuia kulipwa zaidi,  hii ina maana kwamba katika biashara yako ukiwa bora na bidhaa zenye ubora hakuna atakayemzuia  kuuza sana na kupata wateja wengi.

Kama unafanya biashara wekeza muda wako kutafuta buwa bora (excellence). Nguvu zako nyingi uzitumie kutafakari na kujua ni namna gani biashara yako inakwenda kuwa bora.

Uliyeajiriwa katika kampuni au unayefanya kazi serikalini , hakikisha unakuwa bora katika hicho unachokifanya.Muda wako mwingi utumie kufikiri ni namna gani utakuwa bora katika kazi yako.

Mwanafunzi shuleni, usisome tu ili uongoze darasani hapana, soma kwa bidii na huku ukitajua kuwa bora na sio kuwa wa kwanza.
Kama unataka kuwa mtu wa  kwanza darasani hakikisha unakuwa wa kwanza katika ubora.

Elimu yako unayoitafuta hakikisha inakuwa na ubora.Elimu yako itakuwa na umuhimu na watu kukutafuta kufanya kazi na wewe pale utakapokuwa na elimu iliyo bora.

Namna gani ufanye ili kuwa bora!
Hadi hapa tulipofikia unaelewa  na umetambua faida za kuwa bora katika kila unachokifanya.
Sasa ni namna gani unaweza kuwa bora

1.Fanya ubobezi katika jambo/kazi/biashara unayoifanya. Tafuta maarifa zaidi katika biashara yako/kazi yako unayoifanya.
Hakika unatafuta kujua kila kitu kinachohusiana na kazi au biashara yako ili uweze kuifanya katika ubora wa juu zaidi 

2.Ambatana na wale ambao wako vizuri/waliofanikiwa zaidi kwenye kazi husika 
Katika kila kazi/biashara inayofanyika wapo ambao tayari wamekuzidi kiwango fulani.Jifunze kutoka kwao namna gani wanaendesha/kufanya kazi zao na siri ya wao kufika hapo walipo.Hakikisha unajifunza katika kila hatua unayotaka kuifanya kutoka kwao na unakwenda kuwa bora zaidi.

3.Jifunze zaidi kuhusu kazi yako/biashara yako. 
Kadiri ambavyo unakijua kitu vizuri ndivyo ubora wako unavyoongezeka.Hakikisha kila kitu kinachohusika katika baishara yako unakijua vyema. Tafuta kuboresha kila siku na kufikia kwenye ubora unaouhitaji.

4.Soma vitabu vinavyohusu fani /kazi yako
Kama ni biashara tafuta vitabu ambavyo vinafundisha kuhusu biashara visome na yale unayoyapata hakikisha unayatendea kazi.Kusoma tu kunakuwa hakuna maana kama hutayafanyia kazi maarifa unayoyapata.
Kulingana na kazi yako unayoifanya , tafuta na soma vitabu vinavyohusu kazi/huduma unayoitoa

5.Hudhuria  semina, makongamano  mbalimbali yahusuyo kazi yako
Yako makongamano mbalimbali , semina zinazofundisha namna ya kufanya jambo fulani.
Hakikisha unashiriki semina hizo na makongamano hayo ili uweze kuwa bora zaidi katika hicho unachokifanya.

Hatua Ya kuchukua;
Wekeza muda wako zaidi na nguvu zako kujua ni namna gani unaweza kuwa bora katika kazi yako/biashara yako.
Usifanye tu ili umalize, hapana fanya kwa ule ubora unaotakiwa.

Tafuta maarifa zaidi, jifunze zaidi, soma vitabu vingi kadiri uwezavyo, hudhuria semina/makongamano kuhusiana na kazi yako na yote unayoyapata yatendee kazi na utakuwa bora zaidi.

Natumai umejifunza kitu cha msingi sana leo, kichukue na hakikisha unakitendea kazi na unakwenda kuwa bora zaidi.

Chema chajiuza.

KARIBU  KATIKA GROUP LA WHATSAP
Tuna group la whatsap letu la whatsap linaloitwa ELIMU KITAA , ambako huko tunapata nafasi ya kujadili mambo mbalimbali, Kurasa za Mafanikio, Hekima Ya Siku Uchambuzi wa Vitabu.
Karibu sana katika group hili tujifunze kwa pamoja.
Kujiunga tuma SMS kwa njia ya whatsap ikiambatana na jina lako na Neno NIUNGE
mfano; Joshua Golyama , NIUNGE   kwenye namba hii 0764257495. Nawe utaunganishwa na group hili.

Ahsante  sana 

Joshua Golyama



Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUANZA UPYA

  Kuanza upya ni jambo zuri ambalo linawezekana katika maeneo mengi ya maisha yetu, iwe ni kazi, uhusiano, au malengo binafsi. Hapa kuna hatua kadhaa unazoweza kuchukua kuanza upya: 1. Tathmini hali ya sasa Anza kwa kufanya tathmini ya hali yako ya sasa.  Jiulize maswali kuhusu maeneo gani unataka kuboresha au kubadilisha. Je, kuna mambo yanayokukwamisha au kukuzuia kufikia malengo yako? Kuelewa hali yako ya sasa ni hatua muhimu katika kuanza upya. 2. Weka malengo Weka malengo wazi na sahihi. Fikiria kwa kina kile unachotaka kufikia na kuamua hatua za kuifikia.  Malengo yako yanapaswa kuwa ya kusisimua, lakini pia yapaswa kuwa ya kufikika na yanayopimika.  Andika malengo yako na uwaeleze kwa uwazi. 3. Panga mpango wa utekelezaji Panga mpango wa vitendo wa jinsi utakavyotekeleza malengo yako. Tambua hatua ndogo na za kivitendo unazoweza kuchukua ili kufikia malengo yako.  Kwa kila hatua, weka muda uliopangwa na rasilimali zinazohitajika. 4. Jifunze kutokana na uz...

AGRICULTURE 101; KILIMO CHA TEMBELE

Habari   rafiki   mpendwa , Karibu   sana   katika   Makala   hii   Ya   Kilimo   na   Ufugaji Na   leo   tunakwenda   kuangalia   kuhusiana   na   Kilimo   Cha   Tembele. Mboga   nzuri   sana   na   inayopenda   na  kutumiwa   na    watu   wengi   sana   duniani Makala   hii   itakuwa   na   Sehemu/Vipengele   vifuatavyo; 1.Utangulizi 2.Aina za Tembele 3.Faida za Kiafya zitokanazo na Tembele 4.Namna Ya Kuandaaa Shamba 5.Kupanda 6 Kuvuna Karibu     sana    tujifunze   kuhusu    tembele. Kilimo cha tembele Kitaalamu    tembele   hujulikana   kama  ...

KARIBU KATIKA PROGRAM YA ELIMU KITAA(LEARNING SITE)

  Elimu Kitaa Foundation inakukakaribisha Katika Program ya Elimu Kitaa Habari ya kwako rafiki yangu. Bila shaka uko vizuri na unaendelea vyema na majukumu ya kila siku. Naitwa Joshua Golyama  mwanafunzi wa Shahada ya awali ya Sayansi ya Kilimo kwa Ujumla(Bsc.Agriculture General) kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine Cha Kilimo (SUA                                         Mwanzilishi wa Program inayoitwa ELIMU KITAA. Leo ninapenda kukuletea maeneo mbalimbali ambayo unaweza yatembelea na tukajifunza pamoja na mimi. Maeneo hayo utapata nafasi ya kusoma makala ambazo ninaziandika kila siku na kuziweka humo, na tukajifunza kwa pamoja na kupata maarifa zaidi na zaidi. Kwanza kabisa nikupe utangulizi wa maana halisi ya Neno hili ELIMU KITAA. Elimu Kitaa ni program inayohusika na kuandika makala mbalimbali katika mitandao ya Kijamii na kuandaa semina mbalimbali zenye kutupa maarifa muhimu san...