Upo usemi unaojulikana sana katika mahusiano ya kimapenzi "Ukipenda Utakitunza" huu ni usemi ambao unatumika sana katika masuala ya mahusiano;
Ikiwa na maana hii, kwamba kama Kijana anampenda Binti (kijana wa kike) atatumia kila namna kuhakikisha Binti yule anakuwa katika hali nzuri , kwa maana ya kumpendezesha na mambo mengine mengi yanayofanana na hayo.
Usemi huu, una ukweli sana katika maisha ya kila siku, na pengine huwa tunautumia msemo huu bila ya kujua kama zinaweza kutusaidia katika maisha yetu ya Kila siku .
Karibu sana katika Kurasa hii ya Asubuhi ya leo tuweze kujifunza juu ya kufanya kile unachokipenda na kuanza kukifanyia kazi .
Kufanya kitu usichokipenda ni hatari sana
Waliofanikiwa hufanya vile vitu wanavyovipenda. Huwezi kufikia mafanikio makubwa katika Maisha yako kama utashughulika na vile usivyovipenda.
Tafuta kitu/jambo unalolipenda, kisha kifanye hicho.
Penda kazi unayoifanya, Penda masomo yako, na chochote kile unachokifanya
Iko nguvu kubwa sana katika kupenda.
Ukipenda, utajitoa kikamilifu kufanya
Ukipenda , utakithamini na kuitunza
Ukipenda, utahakikisha kinakuwa bora sana
Na utatumia kila unavyoweza kuhakikisha jambo hilo linafanikiwa
Na ukiipenda kazi unayoifanya, hutakubali kazi yako iharibike.
Na kufanya kazi usiyopenda ni kupoteza muda na haitakupa ridhiko la kutoka ndani na huwezi kuona Furaha ya kufanya jambo hilo/kazi unayoifanya.
Kwa wanafunzi wa Shuleni na Vyuoni
Ili mwanafunzi aweze kufaulu vizuri katika mitihani ni lazima kwanza alipende somo husika, na mwalimu anayemfundisha .
Asipolipenda somo hawezi kuelewa na akimchukia/kutokumpenda mwalimu hawezi kumuelewa mwalimu wakati anafundisha na kamwe hawezi kufaulu hilo.
Pale unapokifanya kazi unayoipenda , hautaona ugumu wowote katika kilifanya kazi hiyo. Pale wengine wanapolalamika na ugumu wanaoupata, kwako inakuwa rahisi sana kuifanya kwa sababu ni kazi unayoipenda kuifanya.
Hatua ya kuchukua;
Kijue sasa kile unachokipenda zaidi kukifanya, ambacho hata bila kulipwa unaweza kukifanya. Kile ambacho hauko tayari kuona kinaharibika. Kazi ile ambayo unatamani iwe bora zaidi.
Baada ya kukijua/kuijua , anza kukifanyia kazi, fanya kwa bidii na jitoe kikamilifu kuifanya.
Tafuta maarifa ili uweze kuwa bora zaidi katika kazi unayoifanya.
Well said
ReplyDeleteShukrani sana
DeleteNice
ReplyDelete