Kila jambo unalolifanya, lifanye kama wajibu, na usifanye ukitegemea kutambuliwa, au kupewa shukrani. Watu wengi wanapata shida sana pale ambapo wanafanya mambo mengi, na hakuna anayeonekana kuwashukuru kwa yale wanayoyafanya. Unajitoa kwa nguvu zako kuhakikisha kila kitu kinakuwa sawa. Fuatilia mifano hii michache ili uweze kupata kile ninachokimaanisha hapa; Mfano wa kwanza; Viongozi mbalimbali tulio nao, wanatumia muda wao mwingi na nguvu nyingi kuhakikisha wale wanaowaongoza wanafika pale wanapotakiwa kuwa. Na hakuna hata mmoja anayetambua mchango wao na nguvu zao walizotumia kuwaongoza. Na pengine asiwepo hata mmoja wa kusema asante kwa yale wanayafanya. Mfano wa Pili ; kwenye mahusiano,unakuta boyfriend/girlfriend anafanya kila anachoweza ili kuboresha mahusiano yao, kumsaidia kwa kila hali/changamoto anayoipitia Lakini haoni mwenzie akimshukuru au kutambua kwa kile anakifanya. Mfano wa tatu; Kazini kwako, unafanya kila kitu vile inavyotaki...
Hekima, Maarifa na Ufahamu Wekeza Saidia wengine