Habari rafiki mpendwa;
Ni matumaini Yangu u mzima wa afya na waendelea vyema na majukumu yako ya kila siku.
Karibu sana katika Makala hii Ya Kurasa za Mafanikio,
Hakuna jambo chini ya jua ambalo linashindikana kufanyika.
Ndani yetu ipo nguvu kubwa sana ambayo Mungu ameweka ndani yetu.Na kama mtu ataijua nguvu kubwa iliyopo ndani yake , hakika anakwenda kuwa na Maisha mazuri sana.
UKWELI KUHUSU WEWE.
Unajidharau sana na wakati mwingine kudhani kwamba hauna thamani katika dunia hii.Na unadiriki kusema kwamba umezaliwa kwa bahati mbaya.
Kufanya hivyo unajikosea na kujichelewesha mwenyewe, Hakuna mwanadamu alizaliwa kwa bahati mbaya.
Kila mmoja aliyepo katika dunia hii ameumbwa kwa kusudi Maalumu.
Wewe ni wa thamani sana, na kuumbaa kwako duniani kunadhihirisha kuwepo kwa jambo ambalo linakutaka wewe kulitimiza.
Tambua ya kuwa wewe ni mtu wa tofauti na hakuna anayefanana na wewe katika dunia hii.Na Vile wewe unajiona ni tofauti na uhalisia wako(vile Mungu anakuona)
Mungu kukuumba wewe alikuwa na Makusudi kamili na umezaliwa hapo ulipo, na vile ulivyo ni kutokana na mpango na makusudi yake Mungu.
Ndani yako kuna uwezo mkubwa sana, ambao ukiamua kuutumia unaweza kufanya mambo
makubwa sana katika dunia hii.
makubwa sana katika dunia hii.
Usijidharau na kuanza kujiona kama hufai kuwepo duniani , hapana.
Upo duniani kulitimiza Kusudi La Mungu katika maisha yako.
Mungu alituumba ili tuweze kuwa Watawala, na tunatawala kupitia Vipaji na uwezo ambao Mungu ametupa.
Katika makala ya leo tunakwenda kujifunza nguvu iliyopo katika maamuzi ,
Maisha ni maamuzi , ukiamua unaweza kufanya jambo lolote lile ulitakalo kulifanya na kulikamilisha.
Kila jambo linafanikiwa pale mtu anapoamua.
Licha ya kuwa na kanuni zingine za mafanikio/maisha ya kila siku, usipoamua kuzifanyia kazi huwezi kufika popote
Watu wengi tunatamani kufanya mambo mbalimbali katika maisha haya tuliyo nayo. Mwingine anatamani kuanza biashara , mwingine anatamani kulima , na mwingine kufuga na mambo mengine yanayofanana na hayo.
Changamoto kubwa ni kwa sababu hatujaamua kufanya , tunatamani kufanya lakini hatujaamua kufanya.
Kutamani ni Msingi mkuu wa Mafanikio.
Lakini "Kutamani hakutakuwa na Maana pale tusipoamua"
Usipoamua na kuchukua hatua ya kuanzisha biashara, hakuna biashara itakayofanyika
Usipoamua na kuchukua hatua juu ya jambo fulani , kamwe hatuwezi kufika kule tunataka kufika.
Kiwango cha Maisha yako, kinategemea na Umeamua yaweje,
Ukitaka kuwa Masikini ni wewe tu kuamua
Ukitaka utajiri ni wewe tu kuamua.
Maamuzi yako na wewe, mhusika na bosi wa maisha yako ni wewe.
Hakuna mwingine mwenye dhamana na maisha yako.Usipoamua sasa kutafuta na kufanya bidii ili kuwa na Maisha bora , hutamulaumu yeyote bali ni wewe mwenyewe.
Hauwezi kuwa bora katika fani fulani kama tu hujaamua kwa hivyo(bora)
Hauwezi kufaulu mtihani wako kama haujaamua kufaulu mtihani
Hauwezi kuwa Tajiri kama tu haujaamua kuwa tajiri.
Hivyo amua sasa ni aina gani ya maisha unayahitaji, kiwango gani unataka kufanikiwa na fedha kiasi gani unataka kumiliki n.k.
Na kisha AMUA kuvitafuta kwa bidii zote na hakika utavipata .
Hatua Ya Kuchukua;
Usiishie tu kutamani, bali anza kuchukua hatua.
Amua kuwa bora, kufanya kazi kwa bidii na kutekeleza kile ambacho ulitamani kifanyike katika maisha yako.
Kama kuna kitu unakitamani kukifanya katika maisha yako, amua na anza kukifanya.
Amua na chukua hatua ya Kujifunza zaidi ili kuweza kuwa bora zaidi katika kila jambo unalolifanya hapa duniani .
Ahsante sana kwa wakati wako.
Joshua Golyama .
_____________________________________
Makala hii imeandikwa na ;
Joshua Golyama, ambaye ni Mwalimu, Mtaalamu wa Kilimo na Mifugo, Mhamasishaji Wa Mafanikio na Mwandishi.
+255 764 257 495 / +255 622 163 323
Barua pepe; golyamajoshua@gmail.com
Blogu; elimukitaa2020.blogspot.com
Comments
Post a Comment