Skip to main content

HEKIMA YA SIKU; Usijilazimishe kufanya yasiyo sahihi/usiyoyapenda ili kuwaridhisha/kuwafurahisha wengine.

Habari  rafiki  mpendwa,

 Ni  kawaida  ya  kila  mtu/ mwanadamu   kufanya jambo   ambalo   litawaridhisha   wale wanaolitazama   na   pengine   kusifiwa   pia,   hata kama   jambo   hilo   mtu   hapendi   kulifanya, analifanya   ili   tu   kuwaridhisha   watu   wengine.

Asili   ya   sisi   wanadamu   ni   kwamba,   tunajisikia   furaha   sana   pale   tunapolifanya jambo   na   watu   wengine   kuridhishwa   nalo,   na   mategemeo   yetu   ni   ili   wanadamu   waweze   kutusifia   kwa   kazi   nzuri   ambayo   tumeweza   kuifanya.   Haijalishi   jambo   hilo   ni   sahihi   au   sio   sahihi,   au   tunalipenda   au   hatulipendi 

Ndugu   yangu ,   unachotakiwa   kufahamu   ni   kwamba   si   kila   jambo   utakalolifanya   litawaridhisha   watu   wote,   yapo   mambo mengine   ambayo   hauwezi   kumridhisha   hata mtu   mmoja ,   hii   haimanishi   kwamba   umekosea,   hapana   ila   hawajakuelewa   nini   unachokitarajia   baada   ya   kufanya   jambo   hilo.

Tunatumia   muda   mwingi   sana    na   nguvu   nyingi   sana   kufanya   yale    ambayo yatawaridhisha   watu   wote,    hata   kama hatupendi   kuyafanya   ila   tunafanya   ili   tupate   heshima   na   kusifika.
  
Mfano;   mwanafunzi   anaamua   kusoma kuhusiana   na   fani   fulani , si   kwamba   anapenda   hapana   ila   anafanya     ili   kuwaridhisha   wazazi   wake,   na   pia mke/mume    anafanya   jambo   ili   kumridhisha yule   anayemtazama.

Asubuhi   ya   leo   tambua   neno   hili   kwamba ,   usifanye   jambo   kuwaridhisha   wengine,   fanya lile   ambalo   unalipenda   na   lenye   manufaa   kwako.
Hauwezi   kumridhisha   kila   mtu/mwanadamu   kutokana   na   kile   unachokifanya ,    kwa sababu   wao   hawajui   nini   umekiona   baada   ya   kuamua   kulifanya   jambo   lile. 

Ni   hatari   sana   kufanya   jambo   ambalo   sio   sahihi   na   lisilo   na    umuhimu   kwako,    unakuwa   unapoteza   muda   mwingi   sana   kuhusika   na   mambo   yasiyo   na   msaada kwako.
Fanya   yale   ya   muhimu     kwako   na   unayoyapenda   kuyafanya.

Weka   akilini   mwako   kwamba ,  si   kila   utakalolifanya   litampendeza   kila   mtu,   yapo  mengine   yatakataliwa na   kila   mtu   na   si kwamba   sio   sahihi   hapana,   ni   kwamba      wanadamu   hawajazoea   na   hawawezi   kukubali   ufanye   jambo   lilio   tofauti   na   yale tuyafanyayo   kila    siku  

Usiogope    kufanya   jambo    jipya   na   lililo   tofauti   na   mazoea   ya   kila   siku,    kama   umelihakikisha   na   kuona   lina   manufaa makubwa    hapo   baadaye.

Hatua ya kuchukua; 
Kijue   nini   unakitaka   katika   maisha   yako,   na   anza   kufanya   kile    kitakachokuwa   na   manufaa    katika     maisha   yako   na   kukupelekea   kule   ambako   umedhamiria kufika.  Yapo   mambo    magumu   na   yatofauti   utayafanya,   na   pengine    kukosa   msaada   kabisa    kufanikisha   jambo   hilo,   hayo   yasikuvunje   moyo   endelea   mbele   kufikia   pale ulipokusudia.
  
Jua    kuwa   wewe    ni   bosi   wa   maisha    yako na   mhusika   mkuu ,   hivyo    fanya   kila   uwezalo   kuhakikisha   una   yapelekea   maisha   yako   kule   yanakotakiwa    kufika.



Joshua Golyama.

#Hekima Ya Siku 
_____________________________________________________
Makala hii imeandikwa na ; 
Joshua Golyama, ambaye ni Mwalimu, Mtaalamu wa Kilimo na Mifugo, Mhamasishaji Wa Mafanikio na Mwandishi.

+255 764 257 495 / +255 622 163 323
Barua pepe; golyamajoshua@gmail.com

Blogu; elimukitaa2020.blogspot.com

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUANZA UPYA

  Kuanza upya ni jambo zuri ambalo linawezekana katika maeneo mengi ya maisha yetu, iwe ni kazi, uhusiano, au malengo binafsi. Hapa kuna hatua kadhaa unazoweza kuchukua kuanza upya: 1. Tathmini hali ya sasa Anza kwa kufanya tathmini ya hali yako ya sasa.  Jiulize maswali kuhusu maeneo gani unataka kuboresha au kubadilisha. Je, kuna mambo yanayokukwamisha au kukuzuia kufikia malengo yako? Kuelewa hali yako ya sasa ni hatua muhimu katika kuanza upya. 2. Weka malengo Weka malengo wazi na sahihi. Fikiria kwa kina kile unachotaka kufikia na kuamua hatua za kuifikia.  Malengo yako yanapaswa kuwa ya kusisimua, lakini pia yapaswa kuwa ya kufikika na yanayopimika.  Andika malengo yako na uwaeleze kwa uwazi. 3. Panga mpango wa utekelezaji Panga mpango wa vitendo wa jinsi utakavyotekeleza malengo yako. Tambua hatua ndogo na za kivitendo unazoweza kuchukua ili kufikia malengo yako.  Kwa kila hatua, weka muda uliopangwa na rasilimali zinazohitajika. 4. Jifunze kutokana na uz...

AGRICULTURE 101; KILIMO CHA TEMBELE

Habari   rafiki   mpendwa , Karibu   sana   katika   Makala   hii   Ya   Kilimo   na   Ufugaji Na   leo   tunakwenda   kuangalia   kuhusiana   na   Kilimo   Cha   Tembele. Mboga   nzuri   sana   na   inayopenda   na  kutumiwa   na    watu   wengi   sana   duniani Makala   hii   itakuwa   na   Sehemu/Vipengele   vifuatavyo; 1.Utangulizi 2.Aina za Tembele 3.Faida za Kiafya zitokanazo na Tembele 4.Namna Ya Kuandaaa Shamba 5.Kupanda 6 Kuvuna Karibu     sana    tujifunze   kuhusu    tembele. Kilimo cha tembele Kitaalamu    tembele   hujulikana   kama  ...

KARIBU KATIKA PROGRAM YA ELIMU KITAA(LEARNING SITE)

  Elimu Kitaa Foundation inakukakaribisha Katika Program ya Elimu Kitaa Habari ya kwako rafiki yangu. Bila shaka uko vizuri na unaendelea vyema na majukumu ya kila siku. Naitwa Joshua Golyama  mwanafunzi wa Shahada ya awali ya Sayansi ya Kilimo kwa Ujumla(Bsc.Agriculture General) kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine Cha Kilimo (SUA                                         Mwanzilishi wa Program inayoitwa ELIMU KITAA. Leo ninapenda kukuletea maeneo mbalimbali ambayo unaweza yatembelea na tukajifunza pamoja na mimi. Maeneo hayo utapata nafasi ya kusoma makala ambazo ninaziandika kila siku na kuziweka humo, na tukajifunza kwa pamoja na kupata maarifa zaidi na zaidi. Kwanza kabisa nikupe utangulizi wa maana halisi ya Neno hili ELIMU KITAA. Elimu Kitaa ni program inayohusika na kuandika makala mbalimbali katika mitandao ya Kijamii na kuandaa semina mbalimbali zenye kutupa maarifa muhimu san...