HEKIMA YA SIKU; Usijilazimishe kufanya yasiyo sahihi/usiyoyapenda ili kuwaridhisha/kuwafurahisha wengine.
Habari rafiki mpendwa,
Ni kawaida ya kila mtu/ mwanadamu kufanya jambo ambalo litawaridhisha wale wanaolitazama na pengine kusifiwa pia, hata kama jambo hilo mtu hapendi kulifanya, analifanya ili tu kuwaridhisha watu wengine.
Asili ya sisi wanadamu ni kwamba, tunajisikia furaha sana pale tunapolifanya jambo na watu wengine kuridhishwa nalo, na mategemeo yetu ni ili wanadamu waweze kutusifia kwa kazi nzuri ambayo tumeweza kuifanya. Haijalishi jambo hilo ni sahihi au sio sahihi, au tunalipenda au hatulipendi
Ndugu yangu , unachotakiwa kufahamu ni kwamba si kila jambo utakalolifanya litawaridhisha watu wote, yapo mambo mengine ambayo hauwezi kumridhisha hata mtu mmoja , hii haimanishi kwamba umekosea, hapana ila hawajakuelewa nini unachokitarajia baada ya kufanya jambo hilo.
Tunatumia muda mwingi sana na nguvu nyingi sana kufanya yale ambayo yatawaridhisha watu wote, hata kama hatupendi kuyafanya ila tunafanya ili tupate heshima na kusifika.
Mfano; mwanafunzi anaamua kusoma kuhusiana na fani fulani , si kwamba anapenda hapana ila anafanya ili kuwaridhisha wazazi wake, na pia mke/mume anafanya jambo ili kumridhisha yule anayemtazama.
Asubuhi ya leo tambua neno hili kwamba , usifanye jambo kuwaridhisha wengine, fanya lile ambalo unalipenda na lenye manufaa kwako.
Hauwezi kumridhisha kila mtu/mwanadamu kutokana na kile unachokifanya , kwa sababu wao hawajui nini umekiona baada ya kuamua kulifanya jambo lile.
Ni hatari sana kufanya jambo ambalo sio sahihi na lisilo na umuhimu kwako, unakuwa unapoteza muda mwingi sana kuhusika na mambo yasiyo na msaada kwako.
Fanya yale ya muhimu kwako na unayoyapenda kuyafanya.
Weka akilini mwako kwamba , si kila utakalolifanya litampendeza kila mtu, yapo mengine yatakataliwa na kila mtu na si kwamba sio sahihi hapana, ni kwamba wanadamu hawajazoea na hawawezi kukubali ufanye jambo lilio tofauti na yale tuyafanyayo kila siku
Usiogope kufanya jambo jipya na lililo tofauti na mazoea ya kila siku, kama umelihakikisha na kuona lina manufaa makubwa hapo baadaye.
Hatua ya kuchukua;
Kijue nini unakitaka katika maisha yako, na anza kufanya kile kitakachokuwa na manufaa katika maisha yako na kukupelekea kule ambako umedhamiria kufika. Yapo mambo magumu na yatofauti utayafanya, na pengine kukosa msaada kabisa kufanikisha jambo hilo, hayo yasikuvunje moyo endelea mbele kufikia pale ulipokusudia.
Jua kuwa wewe ni bosi wa maisha yako na mhusika mkuu , hivyo fanya kila uwezalo kuhakikisha una yapelekea maisha yako kule yanakotakiwa kufika.
Joshua Golyama.
#Hekima Ya Siku
_____________________________________________________
#Hekima Ya Siku
_____________________________________________________
Makala hii imeandikwa na ;
Joshua Golyama, ambaye ni Mwalimu, Mtaalamu wa Kilimo na Mifugo, Mhamasishaji Wa Mafanikio na Mwandishi.
+255 764 257 495 / +255 622 163 323
Barua pepe; golyamajoshua@gmail.com
Blogu; elimukitaa2020.blogspot.com
Comments
Post a Comment